ZANZIBAR KUSHIRIKIANA NA CHINA KATIKA UTAFITI NA TAALUMA ZA AFYA
Na Mwandishi Wetu, Zanzibar
WAZIRI wa Afya Zanzibar, Nassor Ahmed Mazrui amesema watashirikiana na Chuo
Kikuu cha Fudan Medical collage cha Shanghai cha nchini China katika masula
mazima ya tafiti na taaluma za afya.
Waziri Mazrui ameyaeleza hayo wakati alipokutana na kufanya mazungumzo na
ujumbe kutoka chuo kikuu cha Fudan Medical collage ambao umefika hapa nchini
kuetembelea sehemu mbali mbali katika sekta ya Afya.
Amesema hivi sasa Chuo na Wizara ya Afya wanamkataba wa kuimarisha masuala
mazima ya tafiti kupitia Taasisi ya utafiti ZAHRI Binguni na katika kuendelea
mbele zaidi, watasaini mkataba mwengine mwezi wa Novemba mwaka huu ya
mashirikiano baina Wizara ya Afya na Chuo kikuu hicho.
Amefahamisha kuwa kutokana na chuo hicho kuwa na hospitali zaidi ya 14
ambazo zinaendeshwa na chuo hicho na wanawataalamu wa kila fani Wizara ya Afya
itahakikisha wanapata fursa za kuwapeleka wafanyakazi kusoma zaidi nchini humo
katika kada mbali mbali.
Alifahamisha kuwa kuja kwa ujumbe utasaidia katika kuongeza mambo mbali
mbali ya kuimarisha sekta afya hapa nchini ambayo yatahusika katika mkataba
huo.
Kwa upande wake Mkuu wa chuo cha Fudan Medical collage cha Shanghai nchini
china Zhenghoug Yuan amesema lengo la kuja hapa nchini ni kuimarisha ushirikino
uliopo baina ya Zanzibar na China sambamba na kuimarisha masula ya tatiti za
kifya na masomo kwa wafanyakazi.
No comments