Breaking News

WAHITIMU KIDATO CHA NNE SINGIDA WAONYWA KUTOJIINGIZA KWENYE VITENDO VIOVU

Mkuu wa Shule ya Sekondari ya Dr. Ali Mohammed Shein, Mwalimu Jackson Anthony Maruma

Meneja Maendeleo na Biashara wa Benki ya NBC Tawi la Singida, Olairivan  Elineema ambaye alikuwa mgeni rasmi akimkabidhi cheti Mhitimu Grace Abdallah kwenye mahafali ya 16 ya wahitimu wa kidato cha Nne katika Shule ya Sekondari ya Dr. Ali Mohammed Shein kwa niaba ya Meneja wa benki hiyo Tawi la Singida mwishoni mwa wiki.

....................................


Imeandaliwa na Dotto Mwaibale, Philemon Solomon (0754-362990)


WAHITIMU wa Kidato cha Nne Shule ya Sekondari ya Dr. Ali Mohammed Shein iliyopo Kata ya Misughaa  Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi mkoani Singida wameambiwa kuwa kumaliza kidato hicho iwe ndio mwanzo wa kuanza maandalizi ya kuendelea na masomo ya elimu ya juu hivyo wakati wakisubiri majibu ya mitihani yao  wasije wakajiingiza kufanya vitendo visivyofaa.

Ombi hilo limetolewa na Meneja Maendeleo na Biashara wa Benki ya NBC Tawi la Singida, Olairivan  Elineema ambaye alikuwa mgeni rasmi akizungumza kwenye mahafali ya 16 ya wahitimu hao kwa niaba ya Meneja wa benki hiyo Tawi la Singida mwishoni mwa wiki.

“Mnaporudi nyumbani yale yote waliyoyakazania walimu wenu kuyaweka kwenye vichwa vyenu yenye maadili mema tunawaomba wadogo zetu msiende kuyaacha,  huko nje kuna kila akili ya mtu kuna wavuta bange kuna wahuni msiende kuwa wamoja wapo. Mkienda kuwa wema amuwasaidii tu wazazi wenu ila hata viongozi wenu na Rais wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan ambaye anaiangaikia nchi mnakuwa mna mrahisishia kazi,” alisema Elineema.

Elineema alisema mbali ya kusaidia viongozi hao pia watakuja kusaidia hadi vizazi vyao vinatakapo kuja ambapo alitoa angalizo kuwa watakapo haribu maisha yao watakuwa wamewaambia wazazi wao kuwa hawataki maisha hivyo watakuwa wamefunga hata furaha za watoto wao ambao wangekuja kuwabariki siku za mbele wakizeeka.

Elineema aliwataka wahitimu hao wasifunge safari ya maisha ambayo wazazi wao wamewaanzishia ambapo aliwasihi pindi watakapotoka shuleni hapo waendelee kuwa na nidhamu ile ile waliyokuwa nayo shuleni na jambo  kubwa na la msingi ni kutoacha kumtaja Mungu kwa kila kitu watakachokuwa wakihitaji kukifanya.

Aidha, Elineema aliwaomba wahitimu hao wasiangalie njia iliyo mbaya badala yake waitazame njia iliyo nzuri siku zote za maisha yao na kuwaeleza kuwa hakuna mzazi ambaye atamuangaikia mtoto wake kuanzia mchanga hadi elimu ya juu na mwishoni aje amuache akiharibiwa bila kufaidi matunda yake.

Diwani wa Kata hiyo, Selemani Musa, aliwaomba wazazi na walezi kujenga tabia ya kutoa chakula kwa ajili ya lishe  kwa wanafunzi wa shule hiyo wanapokuwa shuleni.

“Tujitahidi kuwa changia watoto wetu liche wakiwa shuleni ili waweze kusoma kwa mfululizo na bila ya kukosa chakula,” alisema Musa.

 Alisema kuwatunza wanafunzi hao na kuwapa chakula kutawafanya wanafunzi kufanya vizuri kwenye masomo yao ambapo aliomba utaratibu huo wa chakula uanzie shule za msingi.

Mkuu wa Shule hiyo, Jacksom Maruma akizungumza wakati akitoa taarifa ya shule hiyo alisema imeongeza ufaulu wa wanafunzi ambapo kwa mwaka 2023 ufaulu uliongezeka na  kufikia asilimia 96.

Akizungumzia miundombinu alisema walipata msaada wa fedha za Uviko 19 ambapo walipata madarasa mawili na chumba kimoja cha darasa kutoka fedha Serikali Kuu  ambapo pia waliwezeshwa fedha kwa ajili ya ujenzi wa chumba kimoja cha maabara na ujenzi wa matundu 10 ya vyoo ambapo walipata fedha za tozo.

Alisema walipata mifuko 400 ya saruji kwa ajili ya ujenzi wa Hosteli  kupitia kwa aliyekuwa Waziri wa Habari, Mawasiliano, na Teknolojia ya Habari, Nape Nnauye   na kuwa pia wamepokea kompyuta 10, Intanenti routa moja, printa moja kutoka Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote (UCSAF) na kuwa kwa msaada huo wanakila sababu ya kumshukuru Mbunge wa Jimbo la Ikungi Mashariki Miraji Mtaturu na Rais Samia Suluhu Hassan.

Alitaja baadhi ya changamoto kuwa ni uchakavu wa madarasa, hawana ukumbi wa mikutano, samani za maktaba, nyumba za walimu, madarasa chakavu na jengo la utawala.

Akizungumzia kuhusu michezo Mwalimu Maruma alisema wameanzisha kituo cha kuibua vipaji vya mpira wa miguu kinachojulikana kwa jina la Misughaa Sport Centre.

Mwalimu Maruma akizungumzia juu ya chakula kwa ajili ya wanafunzi alishukuru ushirikiano wanaoutoa wazazi kwani wanachakula cha kutosha na kuwa kwenye stoo yao wana akiba ya kutosha chakula ambacho watakitumia hadi mwakani.

Mjumbe wa bodi wa shule hiyo, Fr. Patric Myuku kutoka Jimbo Katoliki Singida aliupongeza uongozi wa shule hiyo, bodi ya shule kwa kazi kubwa wanayoifanya bila ya kuwasahau wahitimu na wazazi.

Fr. Myuku aliwaomba wanafunzi hao wawe wapambanaji na kueleza kuwa maendeleo yanahitaji wanafunzi wanaojibidisha na kuwa wakiwa legelege kwenye masomo hawawezi kufanikiwa na kuwa maisha mazuri kwa asilimia kubwa yanatokana na shule ambapo aliwasisitizia sana washike elimu wasiiache iende zake.

Mwenyekiti wa Bodi ya shule hiyo, Athumani Kitiku alisema katika shule hiyo kuna changamoto nyingi ikiwemo maabara moja, hosteli kwa ajili ya wasichana ambayo itakuwa na uwezo wa kuchukua wanafunzi zaidi ya 100 lakini iliyopo haina uwezo huo hivyo amewaomba wadau na Serikali wawasaidie.

Kwa upande wake Afisa Elimu Sekondari wa Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi, Ngwano John Ngwano aliishukuru Serikali chini ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kutoa fedha zaidi ya Sh. Milioni 136 katika shule hiyo kwa ajili ya ujenzi wa miundombinu  ambapo alihimiza itunzwe.

“Nina imani kuwa Serikali itakapopata nafasi tena tutaweza kupata fedha za kumalizia ujenzi wa maabara ambayo tunayo moja, maboma mawili,” alisema Ngwano.

Aliwahimiza wananchi kuendelea kuchangia chakula cha watoto shuleni  na kueleza kuwa masomo yanakwenda sanjari na chakula.

Wanafunzi wa shule hiyo Shadia Hassan na Ntandu Constantino wakizungumza kwa niaba ya wenzao waliushukuru uongozi wa shule hiyo kwa kuratibu uchangiaji wa chakula shuleni hapo na muitikio wa wazazi wao kwani unawasaidia kupata masomo bila ya kuwa na njaa.

“Tuna mshukuru sana Mkuu wa Shule Jackson Muruma na timu yake pamoja na kamati ya shule kwa mpango wa chakula hapa shuleni umetuusaidia sana na zaidi shukurani zetu tunazitoa kwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuiwezesha shule yetu kupata miundombinu bora kupitia Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi chini ya Mkurugenzi,  Justice Kijazi,” alisema  Shadia Hassan. 

 Afisa Elimu Sekondari wa Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi, Ngwano John Ngwano akizungumza kwenye mahafali hayo.
Diwani wa Kata ya Misughaa, Selemani Musa, akizungumza.
Mwenyekiti wa Bodi ya Shule hiyo, Athumani Kitiku, akizungumzia changamoto kadhaa za shule hiyo.
Mdau wa sekta ya elimu, Fr. Patric Myuku, akitoa nasaha zake kwa wahitimu hao.
Mkuu wa shule hiyo, Jackson Maruma akimkabidhi mgeni rasmi taarifa ya shule hiyo.
Meneja Maendeleo na Biashara wa Benki ya NBC Tawi la Singida, Olairivan  Elineema ambaye alikuwa mgeni rasmi akivikwa skafu mara alipokuwa amefika kwenye mahafali hayo.
Viongozi mbalimbali wakiwa meza kuu wakati wa mahafali hayo.
Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Ikungi,  Ikimbia Nkhangaa (kulia) akiteta jambo na Diwani wa Viti Maalumu, Ester Kimoho wakati wa mahafali hayo.
Mkuu wa shule hiyo, Jackson Maruma akiagana na viongozi mbalimbali waliohudhuria mahafali hayo. Kutoka kushoto ni Fr. Patric Mkuyu, Diwani wa Kata ya Misughaa, Seleman Musa na Meneja Maendeleo na Biashara wa Benki ya NBC Tawi la Singida, Olairivan  Elineema ambaye alikuwa mgeni rasmi.
Meneja Maendeleo na Biashara wa Benki ya NBC Tawi la Singida, Olairivan  Elineema ambaye alikuwa mgeni rasmi, akimkabidhi cheti mmoja wa wahitimu hao wa kidato cha Nne.
Mmoja wa walimu wa shule hiyo akilishwa tamutamu na wahitimu hao.
Wanafunzi wa shule hiyo wakiwa kwenye mahafali hayo.
Muonekano wa akiba ya chakula kwa ajili ya wanafunzi wa shule hiyo.
Wanafunzi wa shule hiyo wakitoa burudani ya ngoma ya asili ya kabila la Wanyaturu wakati wa mahafali hayo.
Mjumbe wa Bodi wa shule hiyo ambaye alikuwa Mshereheshaji mkuu wa mahafali hayo, Fidelis Yunde akiwajibika ipasavyo.
Mwalimu Steven Mwakisole ambaye alikuwa mshereheshaji namba mbili akiwajibika ipasavyo wakati wa mahafali hayo.

Wahitimu wakiwa kwenye mahafali hayo.
Viongozi wakiwa kwenye picha ya pamoja. Kutoka kulia ni Mkuu wa shule hiyo. Jackson Maruma, Mwenyekiti wa Bodi ya shule hiyo, Athumani Kitiku, Meneja Maendeleo na Biashara wa Benki ya NBC Tawi la Singida, Olairivan  Elineema ambaye alikuwa mgeni rasmi na Diwani wa Kata ya Misughaa, Selemani Musa.
Taswira ya mahafali hayo.
Wapiga picha wa kujitegemea wakichukua matukio mbalimbali.
Mwanafunzi wa kidato cha tatu wa shule hiyo, Brayan Amnaay akionesha umahiri wa kugani mashairi
Mahafali yakiendelea.
Burudani zaidi zikiendelea.
Mashairi yakiimbwa.



Skauti wakionesha jinsi ya kupita katika daraja walilolitengeneza kwa kujipanga wao kwa wao

Kijana wa Skauti akionesha umahiri wa kupita kwenye kamba.
Wahitimu wakiwa na vyeti vyao baada ya kukabidhiwa.
Mwanafunzi Shadia Hassan akitoa shukurani kwa niaba ya wanafunzi wa shule hiyo

Picha ya pamoja viongozi mbalimbali, wahitimu na mgeni rasmi, Meneja Maendeleo na Biashara wa Benki ya NBC Tawi la Singida, Olairivan  Elineema.

Vijana wa Skauti wakiongoza maandamano wakati wa mahafali hayo.
Vijana wa Skauti wakiwa tayari kwa mahafali hayo.
Mhitimu wa shule hiyo mwaka 2019, Yasini Itambu, anayesomea Utaalamu wa Miamba ya Madini Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM) akitoa nasaha zake kwa wahitimu hao wazingatie masomo. 
Muonekano wa maabara ya shule hiyo.
Ulinzi ulivyoimarishwa wakati wa mahafali hayo.

Muonekano wa baadhi ya majengo ya shule hiyo.

No comments