Breaking News

KATIBU TAWALA BUKOBA MJINI, KAMATI YA ULINZI NA USALAMA WAINGIA MTAANI KUFANYA USAFI .

Katibu Tawala (DAS) Wilaya ya Bukoba Bi. Proscovia Mwambi akifanya usafi katika maeneo ya Bukoba mjini ikiwa ni utaratibu waliojiwekea wa kufanya usafi kila Jumamosi ya kila mwisho wa mwezi kama Serikali ilivyoagiza.

............................................... 

Na Mwandishi Wetu, Bukoba

KATIBU Tawala (DAS) Wilaya ya Bukoba Bi. Proscovia Mwambi akiambata na wajumbe wa kamati ya ulinzi na usalaam wa wilaya hiyo  kwa kushirikiana na viongozi wengine wamefanya usafi wa mazingira katika maeneo mbalimbali wilayani humo

Shughuli hiyo ya kufanya usafi imefanyika  Februari 22, 2025 kwa kushirikiana na wananchi.

Akizungumza baada ya kufanya usafi usafi huo Mwambi alisema wamefanya usafi huo kwa lengo la kuweka mazingira bora ndani ya wilaya hiyo jambo ambalo litasaidia kuepuka uwezekanp wa kupata magonjwa ya mlipuko kama vile ykuumwa matumbo na kipindupindu.

“ Zoezi hili la kufanya usafi ni endelevu na Serikali ya Wilaya chini ya Mkuu wa Wilaya yetu ya Bukoba Mhe. Erasto Sima imekua ikikisisitiza juu ya utunzaji wa mazingira hivyo ni wajibu kwa kila mmoja wetu kufanya usafi,” alisema Mwambi.

Mwambi alisema kila Jumamosi ya kila mwisho wa mwezi, wanatakiwa kufanya usafi kama Serikali ilivyoagiza na kueleza kwamba Wilaya ya Bukoba kwa mazingira safi inawezekana.

Katibu Tawala (DAS) Wilaya ya Bukoba Bi. Proscovia Mwambi na wajumbe wa kamati ya ulinzi na usalama wakiwa katika picha ya pamoja baada ya kufanya usafi.
Katibu Tawala (DAS) Wilaya ya Bukoba Bi. Proscovia Mwambi akiendelea kufanya usafi.
Usafi ukifanyika.
 

No comments