MAHAKAMA YA TANZANIA KUENDELEA KUIMARISHA UPATIKANAJI WA HAKI
Mkuu wa Wilaya ya Ilala, Edward Mpogolo ambaye alikuwa mgeni rasmi kwenye Maadhimisho ya Siku ya Sheria Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam yaliyofanyika Februari 3, 2025 katika viwanja vya Mahakama Kuu jijini Dar es Salaam akiwa katika picha ya pamoja na Waheshimiwa Majaji. Katikati ni Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam, Salma Mussa Maghimbi, aliyeongoza maadhimisho hayo.
..........................
Na Dotto Mwaibale, Dar es Salaam
MAHAKAMA ya Tanzania inaendelea kuimarisha upatikanaji wa haki kwa kuja na maboresho na mikakati kabambe kuelekea Dira ya Taifa 2050.
Hayo yamebainishwa na Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam, Salma Mussa Maghimbi wakati akisoma hutuba yake kwenye maadhimisho ya Siku ya Sheria yaliyofanyika Februari 3, 2025 katika viwanja vya Mahakama Kuu jijini Dar es Salaam.
Alitaja baadhi ya uimarishaji huo ni pamoja na kuongeza wigo wa upatikanaji
wa huduma za haki kwa wananchi wote, hasa wanaoishi vijijini, kwa kuendelea
kuboresha miundombinu hususani Mahakama za mwanzo, na matumizi ya mifumo ya
kielektroniki ili kufikia watu ambao hawana huduma ya mahakama.
Alitaja
eneo lingine kuwa ni kuimarisha matumizi ya njia mbadala za
utatuzi wa migogoro kwa kuimarisha usuluhishi na upatanishi, hususani migogoro
ya biashara na uwekezaji ambapo Mahakama ya Tanzania
ilianzisha kituo cha Usuluhishi ngazi ya Mahakama Kuu pamoja na kuzitaka
Mahakama zote kuwa na ngazi hiyo kabla ya shauri la madai kusikilizwa kwa njia
za kimahakama.
„ Suala la usuluhishi ni muhimu tukalipa nafasi kubwa katika kwa ngazi zote za Mahakama kwa kuwa linaleta matokeo chanya baina ya pande zote mbili za mgogoro, pia linapunguza gharama pamoja na muda wa kumaliza mashauri kwa wakati na kuwezesha wananchi kuendelea na shughuli zao za kiuchumi, pia kuendeleza kuwepo kwa mahusiano mazuri baina ya pande zote mbili” alisema Jaji Maghimbi.
Jaji Maghimbi alitaja eneo lingine la
uimarishaji ni uboresha sheria, kanuni na taratibu za upatikanaji wa haki, ili
kupunguza muda wa mchakato wa upatikanaji wa haki na kutengeneza mifumo thabiti
ya ufuatiliaji na tathmini ili kuhakikisha uwajibikaji.
Akizungumzia
eneo la kuongeza Matumizi ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA) na
kuongeza Ufanisi katika utoaji huduma
za Mahakama alisema ni kuwa na
mifumo ya Mahakama inayoaminika na kupatikana, yenye ufanisi, uwazi na usalama
kwa watumiaji kwa kuwa na Mahakama
inayotumia teknolojia ya kisasa katika shughuli zake zote na kwa ngazi zote za
Mahakama.
Akizungumzia mahakama kuongeza
imani ya wananchi alisema ni kuimarisha
mifumo ya ushirikishwaji wa wadau kwa kuweka mfumo madhubuti wa kushughulikia mrejesho
kutoka kwa wananchi na kuongeza mikakati ya utoaji wa elimu kwa wananchi kuhusu
taratibu za upatikanaji wa haki.
Jaji Mghimbi akizungumzia
kuimarisha uwezo wa rasilimali watu alisema ni kuweka mikakati ya kuhakikisha kuwa Mahakama
ina watumishi wa kutosha kuendana na mzigo wa kazi kwa kuweka mikakati ya kuongeza motisha kwa watumishi
wa Mahakama ili kuongeza tija na ufanisi, kutoa fursa za kujiendeleza kitaaluma
na mafunzo endelevu kwa watumishi.
Alisema hayo yote yanafanyika ili kumwezesha mwananchi kuendelea
na shughuli zake kwani ilizoeleka kwamba mtu anapokuwa na shauri Mahakamani
huacha kazi zake zote na kuhudhuria mahakamani akifuatilia shauri lake lakini
kwa sasa anaweza kufuatilia shauri lake akiwa sehemu yoyote inachotakiwa awe sehemu
yenye mtandao anaweza kuingia katika Mahakama mtandao kisha akaangalia tarehe
ya shauri lake na kile kilichojiri Mahakamani au mwenendo uliokuwepo na
uliofikia Mahakamani hili linamwezesha mwananchi kuona uwazi na kuongeza uwajibikaji
na weledi.
Jaji Maghimbi akizungumzia Nafasi ya Taasisi Zingine Zinazosimamia Haki
Madai katika Kutekeleza Malengo ya Dira 2050 na Nafasi
ya ofisi ya Mwanasheria Mkuu na Wakili Mkuu wa Serikali katika Kusimamia Haki
Madai katika Kufikia Dira ya Taifa ya Maendeleo, 2050 alisema Ofisi hizo mbili ni wadau wakubwa katika kusimamia haki
madai na zina wajibu mkubwa kusimamia mashauri yote ya madai yanayofunguliwa na
serikali dhidi ya mtu, taasisi au kampuni yoyote au madai yanayofunguliwa na
serikali ambapo ofisi hizo huwa pia miongoni mwa wadaawa.
Alisema zina majukumu
makubwa ya kuhakikisha haki madai zinafikiwa kwa wakati kwa kuishauri serikali kutatua
migogoro ya kimadai kwa njia ya suluhu.
Alisema katika kutimiza Dira ya Taifa 2050 ni muhimu
sana mashauri kusikilizwa kwa njia rahisi na zisizomchukulia muda mwingi
mwananchi hivyo kuwepo kwa ofisi hizo mbili zinarahisisha kuhakikisha kuwa
serikali haiwi chanzo cha kukwamisha mashauri yuanayoweza kumalizwa kwa muda
mfupi tena kwa njia rahisi.
Akizungumzia Kuendesha
mashauri ya Madai kwa niaba ya serikali alisema kwakuwa mashauri ya madai wakati mwingine yanahitaji
ufundi wa kisheria ofisi hizo mbili zimekuwa zikitumiwa katika mashauri hayo
hii inasaidia kutokwama kwa mashauri kwa kutokuwepo kwa wataalamu wa sheria
hivyo kuwepo kwa ofisi hizo kunawezesha haki madai kusimamiwa kwa misingi ya
kisheria.
” Nazipongeza ofisi hizi mbili kwa namna ambavyo wanashirikiana na Mahakama katika kuhakikisha haki inapatikana kwa wakati,” alisema Jaji Maghimbi.
Akizungumzia Nafasi na Mchango wa Mawakili wa Kujitegemea Katika Kusimamia Haki Madai Katika Kufikia Dira ya Taifa ya Maendeleo, 2050 alisema Mawakili wa kujitegemea ni wadau wakubwa sana katika kufikia Dira ya Maendeo 2050 katika haki madai.
Alisema Mawakili wa Kujitegemea mara nyingi ndio wanaowashauri wananchi kufungua madai, kuandaa nyaraka za kufungua shauri, kufungua shauri, kushauri kusuluhisha mgogoro kwa njia ya suluhu muafaka ndani au nje ya Mahakama.
” Iwapo Mawakili wa Kujitegemea watatekeleza majukumu yao kwa weledi inawezekana kupunguza mashauri Mahakamani hususani yanayofunguliwa bila kuwepo na dai la msingi.” alisema Jaji Maghimbi.
Jaji Maghimbi alisema Mawakili wa kujitegemea wanao wajibu mkubwa wa kuwashauri kutumia njia mbalimbali za utatuzi wa migogoro bila kupotosha hili litasaidia sana wananchi kuwa tayari kukubali migogoro yao kumalizwa kwa wakati na kusema kuwa analisema hilo kwa kuwa wakati mwingine wananchi huamini njia moja ya utatuzi wa migogoro Mahakamani kwa kushauriwa au kuelezwa na hawa wawakilishi wa kisheria.
Jaji Maghimbi akihitimisha hutuba yake akisisitiza uzingatiaji umuhimu wa
upatikanaji wa haki katika maendeleo ya kiuchumi na kijamii, Mahakama ya
Tanzania na taasisi zote zinazoshiriki katika mnyororo wa utoaji wa haki madai
na jinai zina nafasi kubwa kuweka mikakati haina budi kutekelezwa ipasavyo ili
kuwezesha kufikiwa kwa malengo yaliyowekwa katika sekta zote za kiuchumi na
kijamii na kuwa na taifa jumuishi, lenye ustawi, haki, na linalojitegemea
kufikia 2050 kwa kutokomeza umaskini wa
aina zote, na kujenga taifa lenye uchumi imara, jumuishi, na shindani
utakaoboresha maisha ya watu.
Aidha Jaji Maghimbi alikumbusha umma kuwa kauli mbiu ya maadhimisho hayo kuwa ni endelevu na itaishi kwa mwaka mzima hivyo mambo mbalimbali yataendelea kufanyika kwa kuzingatia kauli mbiu hiyo.
Jaji Maghimbi ameendelea kuwasihi Majaji,
Mahakimu, Waamuzi wote pamoja na Mawakili wa serikali na wale wa kujitegema kuhakikisha
wanafanya kazi kwa kuzingatia sheria, kanuni na taratibu ili kuimarisha imani
ya Wananchi kwenye vyombo vya utoaji haki pamoja na utii wa Sheria kwa ujumla
ambavyo ndio vitasimamia nchi yenye haki na kufanikisha kufikia malengo makuu
ya Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050. Kauli Mbiu ya Maadhimisho hayo ni Tanzania ya 2050: Nafasi ya Taasisi zinazosimamia haki madai katika
No comments