TAMUFO YAWAPONGEZA VIONGOZI WALIOTUNUKIWA TUZO YA BALOZI WA AMANI DUNIANI
Katibu Mkuu wa Umoja wa Wanamuziki Tanzania (TAMUFO) na Balozi wa Amani Stella Joel,akizungumza wakati wa hafla ya kutunuku Tuzo ya Ubalozi wa Amani Duniani kwa Viongozi mbalimbali.
......................................
Na Dotto Mwaibale, Dar es Salaam
UMOJA wa Wanamuziki Tanzania (TAMUFO), kupitia viongozi wa
umoja huo wamewapongeza mabalozi wote waliotunukiwa hadhi ya
Balozi wa Amani Duniani (AMB) "Peace Ambassador (AMB)" na
Greenling Peace Foundation.
Tuzo hizo zilitolewa na Mwenyekiti Mwanzilishi wa Greeling Global Peace
Organization Zambia Prof Bishop Kennedy Songwe pamoja na mgeni rasmi wa hafla
ya utoaji wa tuzo hiyo Balozi Prof. Askofu Rejoice Ndalima.
Katika hafla ya kutunuku tuzo hizo iliyofanyika Ukumbi wa
Rungwe Hotel Jijini Dar es Salaam, ilihudhuriwa na wageni waalikwa, wawakilishi
wa taasisi mbalimbli, wanaharakati wa amani na viongozi wa kimataifa.
Viongozi wa TAMUFO ambao ni Mabalozi wa Amani walitumia nafasi hiyo kuwapongeza wadau na Viongozi hao ambao ni mabalozi wa Amani kwa kutunukiwa hadhi hiyo jambo ambalo ni la kujivunia.
Akizungumza katika Kongamano na hafla hiyo Balozi wa Amani Stella
Joel ambaye ni Katibu Mkuu wa TAMUFO alihimiza Watanzania kuendelea kuilinda amani
ya nchi yetu kwa nguvu zetu zote.
Alisema Upendo ni Amri iliyo kuu tuliyopewa na Mwenyezi
Mungu kila Mtanzania anapaswa kuwa na upendo kwani matunda ya Upendo ni Amani
Uvumilivu, Utu Wema na mambo yote yaliyo ya haki.
“Tuitafute haki pasipo kushindana jambo litakaloifanya nchi
yetu iendelee kustawi kwa kudumisha upendo, amani na mshikamano wa kitaifa,” alisema Joel.
Kwa upande wake Balozi wa Amani Dkt. Frank Richard ambaye ni
Mlezi wa TAMOFO alisema katika kongano hilo watu 11 walitunukiwa Tuzo za Ubalozi wa Amani wakiwemo Viongozi wa Dini baada ya kutambuliwa
kutokana kuhamasisha kudumisha amani bila ya kuchoka.
Naye Mkurugenzi wa
Makumbusho ya Viumbe Hai Iliyopo jijini Arusha Dkt. Christina
Ngereza amewahimiza Watanzania kuendelea kudumisha utamaduni wetu
tuliodumu nao kwa muda mrefu wa kuitunza amani yetu badala ya kujiingiza kwenye
mambo ya kigeni hasa kwa kundi la
vijana.
“ Tutunze heshima na miiko tuliofundishwa na wazee wetu ambayo ni kupendana kuheshimiana na hivyo
kudumisha Amani na Utulivu katika nchi yetu,” alisema Dkt. Ngereza.
Baadhi ya viongozi waliotunukiwa tuzo hiyo ni Balozi Dkt.
Jacob Mutashi, Balozi Dkt. Gideon Lukindo, Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa
Uhifadhi wa Shirika la Hifadhi za Taifa Tanzania (TANAPA), Balozi Dkt. Noelia Ansgary Myonga na Mrakibu
wa Polisi (SP), Dkt. Ezekiel Kyogo.
TAMUFO ni mdau na mshirika wa makundi mbalimbali
yanayohamasisha kudumisha amani nchini.
Picha ya pamoja na viongozi waliotunukiwa Tuzo.
Picha ya pamoja.
Brass Bend ya Jeshi la Kujenga Taifa (JKT), iliyokuwa ikitoa burudani wakati wa utoaji wa Tuzo hizo.










.jpg)




No comments