Breaking News

RAIS DKT. SAMIA ALIVYOTEMBELEA MIRADI MBALIMBALI MKOA WA RUKWA NA KUWEKA JIWE LA MSINGI

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akivuta kitambaa kuashiria uzinduzi vihenge na maghala ya kisasa ya kuhifadhia nafaka ya Wakala wa Taifa wa Hifadhi wa Chakula (NFRA), Kanondo, Sumbawanga Mkoani Rukwa tarehe 16 Julai, 2024. 

Uzinduzi wa Vihenge na maghala ya kuhifadhia nafaka ukifanyika.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akibonyeza kitufe kuashiria ununuzi wa nafaka kwa msimu wa 2024-2025 mara baada ya uzinduzi wa vihenge na maghala ya kisasa ya kuhifadhia Nafaka ya (NFRA), Kanondo, Sumbawanga Mkoani Rukwa katika muendelezo wa Ziara yake ya Kikazi mkoani humo.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akizungumza na wananchi mara baada ya kuzindua vihenge na maghala ya kisasa ya kuhifadhia nafaka ya Wakala wa Taifa wa Hifadhi wa Chakula (NFRA) Kanondo, Sumbawanga Mkoani Rukwa. 
Muonekano wa Vihenge na maghala ya kisasa ya kuhifadhia nafaka ya Wakala wa Taifa wa Hifadhi wa Chakula (NFRA) yaliyopo Kanondo, Sumbawanga Mkoani Rukwa.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akivuta kitambaa kuashiria uwekaji wa jiwe la Msingi ujenzi  wa Chuo cha Ufundi Stadi na Huduma (VETA) cha Mkoa wa Rukwa kilichopo Kata ya Momoka, Sumbawanga. 

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akivuta kitambaa kuashiria uzinduzi wa Majengo ya Chuo cha Ualimu Sumbawanga Mkoani Rukwa. 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha na viongozi mbalimbali, Wanafunzi na Wakufunzi wa Chuo cha Ualimu Sumbawanga Mkoani Rukwa

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiteta jambo na Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Mhe. Profesa Adolph Mkenda wakati akimuonesha Majengo ya Chuo cha Ualimu Sumbawanga yaliyopo Kata ya Momoka. 
Taswira ya Majengo ya Chuo cha Ufundi Stadi na Huduma (VETA) Mkoa wa Rukwa kilichopo Kata ya Momoka, Sumbawanga. 

No comments