Breaking News

ASAS MZALENDO ANAYECHOCHEA MAENDELEO MKOANI IRINGA

Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (MNEC) Mkoa wa Iringa, Salim Abri Asas, akihutubia katika moja ya mikutano yake mkoani humo.

--------------------------------

Na Dotto Mwaibale


UZALENDO ni hali ya mtu kuipenda, kuithamini na kujitoa kwa ajili ya nchi na  Mzalendo wa kweli wakati wote anaweka maslahi ya nchi na ya jamii mbele.

 

Uzalendo unabeba dhana pana ikianzia asili, utamaduni, lugha, siasa, historia zote zikifungwa kwenye dhana kuu ya utaifa.


Katika Taifa la Tanzania kumekuwepo na wazalendo wengi, baadhi wamekwisha tangulia mbele za haki akiwemo aliyekuwa Rais wa Kwanza wa Tanzania Hayati Julius Kambarage Nyerere, Hayati Abeid Amani Karume, Hayati Rashid Mfaume Kawawa, Hayati Edward Moringe Sokoine, Hayati Edward Ngoyai Lowassa, Hayati Bibi Titi Mohamed na wengine wengi.

Leo napenda kumuongelea Salim Abri Asas ambaye ni  Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (MNEC) Mkoa wa Iringa.


Kazi kubwa anayoifanya Asas Mkoa wa Iringa katika kuimarisha Chama Cha Mapinduzi (CCM) na kujitolea kwenye masuala ya kijamii ni kubwa mno na inaonekana na kila mpenda maendeleo mkoani humo na nchini kwa ujumla.


 MNEC huyo amefanya mengi na anaendelea kuyafanya bila ya kubagua makundi ya watu na hiyo ni kwa sababu ya hofu ya Mungu aliyonayo.


Asas ambaye ni mfanyabiashara mkubwa wa mazao yanayotokana na ng’ombe  kupitia kampuni yake ya ASAS DAIRIES amekuwa akichagiza maendeleo kwa makundi mbalimbali na Chama Cha Mapinduzi (CCM) na jumuiya zake.


Kuimarisha uhai wa chama, Asas amefanya makubwa kwani kwa nyakati tofauti alitoa Sh.Milioni 13 kwa ajili ya kusaidia maendeleo ya Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) Mkoa wa Iringa.


Asas hakuishia hapo, alitoa tena Sh. Milioni 5 kwa UWT Wilaya ya Kilolo kwa ajili ya kusaidia ujenzi wa ukumbi.

Kutokana na moyo wake wa kizalendo, Asas  ametoa msaada wa simu janja 36 kwa chama hicho Wilaya ya Mufindi alizosema zitumike kwa ajili ya usajili wa wanachama kidigitali katika kata zote.

Kwenye makundi ya kijamii Asas kupitia kampuni yake alitoa Sh.Milioni 100 kusaidia wafanyabiashara ndogondogo wa Iringa ili zitumike kujenga vibanda vya kufanyia biashara zao.

Hiyo ni baadhi ya michango kati ya mingi ambayo Asas amekuwa akiitoa kutokana na uzalendo alionao kwa Taifa lake la Tanzania.

Pamoja na kuwa kinara wa kuchagiza maendeleo ya wana Iringa na CCM pia amekuwa mkali pale anapoona mambo hayaendi vizuri.

MNEC huyo amekuwa akikemea vitendo vya rushwa wakati wa chaguzi ambapo kwa nyakati tofauti amekuwa akisema viongozi wanaopatikana kwa kununuliwa hawawezi kuwatumikia wananchi.

Asas katika kuhimiza uimarishaji wa chama hicho alisema hakuna mtu atakayetoka nje  atakayefanya kazi hiyo bali kitajengwa na wanachama wenyewe kwa kuwa wazalendona kujitoa.

Aidha, katika kuimarisha uhai wa chama mfanyabiashara huyo amekuwa akifanya ziara za kikazi kwenye wilaya zote na kuhimiza suala la kuwatumikia wananchi na kuwaletea maendeleo.

Mbali ya kazi kubwa anayoifanya pia amekuwa akishiriki katika matukio ya kitaifa yanayofanyika mkoani humo yakiwemo ya mbio za Mwenge wa Uhuru, uhamasishaji wa kutunza mazingira na mengine yanayofanana na hayo.

 

Kwa leo nakomea hapa,  nakutakia kazi njema Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (MNEC) Mkoa wa Iringa, Salim Abri Asas ya kuwatumikia wana Iringa na Taifa kwa ujumla. Kazi Iendelee.Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (MNEC) Mkoa wa Iringa, Salim Abri Asas, akiweka jiwe la Msingi la Ujenzi wa Ofisi ya CCM Kata ya Upendo.

Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi Taifa (MNEC),  Salim Abri Asas  akizindua ujenzi wa ofisi ya CCM Kata ya Kiyowela

MNEC Mkoa wa Iringa Salim Abri akihutubia maelfu ya wanannchi katika moja ya mikutano yake mkoani humo.Wafanyakazi wa Kampuni ya Asas na madiwani wa Iringa wakitoa msaada kwa watoto wenye uhitaji.

Mkuu wa Wilaya ya Iringa Kheri James (wa pili kushoto) , Mkurugenzi wa Kampuni ya mafuta ya ASAS Energy Ahmed Abri (kushoto) na Kiongozi Mkuu wa mbio za mwenge Kitaifa Godfrey Mzava wakifuatilia Mradi wa kituo Cha Mafuta. 

No comments