ASASI ZA KIRAIA ZAIOMBA SERIKALI KUHAKIKISHA MAKUNDI MAALUM YANAWEZESHWA
Meneja Programu wa FCS Bi. Nasim Losai akizungumza na waandishi wa Habari katika mkutano wa kitaifa wa watu wenye ulemavu, madiwani na wadau, uliofanyika Agosti 12, 2024 Jijini Dar es salaam.
.......................
Na Mwandishi Wetu
Asasi za Kiraia nchini kupitia Shirika la The Foundation for Civil Society
(FCS), imeiomba Serikali iangazie katika kuhakikisha makundi maalum
yanawezeshwa kufikia miundombinu ya kidigitali ili waweze kushiriki katika
michakato ya maendeleo na kujiimarisha kiuchumi.
Hayo yamesemwa na Meneja Programu wa FCS Bi. Nasim Losai katika mkutano wa
kitaifa wa watu wenye ulemavu, madiwani na wadau, uliofanyika Agosti 12, 2024
Jijini Dar es salaam.
Bi. Losai amesema kuwa mkutano huo umejikita katika kuangazia ushiriki wa
watu wenye ulemavu katika maendeleo, uchumi na kijamii, huku ukiangazia
matumizi ya takwimu za sensa katika kuboresha mipango ya halmashauri za wilaya
na ngazi za kata.
Aidha, ameeleza kuwa Serikali imekuwa Sikivu katika kuhakikisha makundi
maalum yanafikiwa na kuwezeshwa katika shughuli za kiuchumi na kujiongezea
kipato, nakwamba FCS wamekuwa wakIisadia serikali katika kuunga mkono juhudi
hizo kutokana na zoefu wao wa zaidi ya miaka 20 ya kufanya kazi na jamii.
"FCS tuna zaidi ya miak 20 tumekuwa tukisaidia serikali hasa katika
shughuli za jamii na kutetea watu wenye ulemavu na michakato ya kiserikali,
hasa kwenye majengo mengi mioundombinu imebadilika na kazi kubwa imefanywa na
FCS pamoja na makundi haya" amsema Bi. Losai.
Kwa upande wake Mshauri wakitalam masuala ya watu wenye ulemavu Tanzania
Peter charlse, amesema mkutano huo umejumuisha watu mwenye ulemavu zaidi ya 600
kutoka ndani ya Jiji la Dar es salaam wakiwepo madiwani 60 wa viti maalimu na
wale wakuteuliwa.
Amesema kuwa malengo ya mkutano huo ni kuwajengea uelewa watu wenye ulemavu
katika masuala mbalimbali na kuangazia zaidi eneo la uchumi na kuona fursa zipi
walemavu wameweza kushirikishwa na ambazo wanaziweza.
"Ushirikishwaji wa watu wenye ulemavu bado ni mdogo ndio maana
tumewaalika madiwani ili kuangalia changamoto zilizopo na kuwajengea ili
kuyaingiza katika mipango yao ya maendeleo kupitia Mabaraza yao ndani ya
halmashauri" amesema.
Naye Mwenyekiti wa Chama cha Walemavu Tanzania Hamadi Abdallah komboza,
amesema changamoto kubwa kwa watu wenye ulemavu ni masuala ya ajira, huku
akimuomba kamshina wa kazi na vyama vyenye ulemavu kufanya ukaguzi kwenye
mashirika na taasisi ambazo zinapaswa kuajiri watu wenye ulemavu lakini bado
hazijatekeleza nakwamba msukumo zaidi unahitajika.
Katibu Mkuu Shirikisho la vyama vya watu wenye ulemavu Tanzania, Jonas
Lubalo ameishukuru taasis ya Ikupa Trust Fund kwa kuendelea kuchangia na kutoa
huduma kwa watu wenye ulemavu katika maeneo mbalimbali hapa nchini
No comments