Breaking News

RC DANIEL CHONGOLO AZINDUA AWAMU YA PILI YA BODI YA PAROLE YA MKOA WA SONGWE

Mkuu wa Mkoa wa Songwe, Mheshimiwa Daniel Chongolo, akiwa katika picha ya pamoja na Wajumbe wa Bodi ya Parole baada ya kuizindua bodi hiyo Septemba 17, 2024.

...............................

Na Mwandishi Wetu, Songwe. 

MKUU wa Mkoa wa Songwe, Mheshimiwa Daniel Chongolo, amezindua rasmi awamu ya pili ya Bodi ya Parole ya mkoa wa Songwe. Uzinduzi huo umefanyika baada ya muda wa bodi ya awali kumalizika mwaka 2023, ambapo bodi hiyo hudumu kwa kipindi cha miaka mitatu tangu kuanzishwa kwake hadi kuundwa kwa bodi mpya.

Hafla ya uzinduzi wa Bodi hiyo Imefanyika jana katika ukumbi wa Mpende, jirani na Halmashauri ya Wilaya ya Mbozi, na imehudhuriwa na RPO SACP John F Daud kamishna msaidizi mwandamizi wa jeshi la magereza pamoja na wadau mbalimbali wa sekta ya sheria na urekebishaji wa wafungwa. Bodi hiyo inalengo la kuwasaidia wafungwa ambao wanakidhi vigezo vya kutumikia kifungo cha nje ya gereza, hatua inayolenga kusaidia kuwarudisha wafungwa hao kwenye jamii kwa taratibu za kisheria.

Aidha Mhe. Chongolo amepongeza juhudi za bodi katika kuhakikisha haki inatendeka kwa wafungwa wanaostahili, na amesisitiza umuhimu wa bodi hiyo katika kuboresha utekelezaji wa majukumu ya bodi . Bodi mpya inatarajiwa kuendeleza mchakato wa kupunguza msongamano gerezani kwa kuwaruhusu wafungwa wenye sifa kutumikia vifungo vya nje chini ya uangalizi maalum.

Bodi hiyo inatarajiwa kuleta ufanisi zaidi katika utekelezaji wa majukumu ya Bodi ya Parole kwa kipindi cha miaka mitatu ijayo.

Mkuu wa wa Mkoa wa Songwe, Mheshimiwa Daniel Chongolo, akizungumza na wajumbe wa bodi hiyo baada ya kuizindua rasmi.

No comments