KATIBU CCM MKOA WA PWANI: MSIWAPOTEZE VIONGOZI WAZURI KWA SABABU YA CHUKI ZENU ZA MAJUMBANI
Mkutano wa ndani ukifanyika
..............................
Na Mwandishi Wetu
Viongozi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Pwani wameaswa kutowapoteza viongozi wazuri katika mchakato wa
uchaguzi wa Serikali za Mitaa kutokana na chuki zao binafsi.
Hayo yamesemwa na Katibu wa CCM Mkoa wa Pwani, Kitte Adam Mfilinge
wakati alipokuwa akiongea katika Mkutano wa ndani na viongozi wa Halmashauri
Kuu ya CCM, Mabaraza ya Jumuiya za CCM
na wazee maarufu uliofanyika leo tarehe 18/09/2024 katika ukumbi wa
Pentagon ulioko Mlandizi Wilaya ya Kibaha Vijijini.
Kitte amesema wako viongozi ambao
wanagombana majumbani kisha wanatumia nafasi
hiyo kuleta magonvi kwenye vikao na kukata majina ya watu ambao wangefaa
kuwa Viongozi.
" Msiwapoteze viongozi wazuri kwa sababu ya chuki zenu za
majumbani" Kitte
Amesema unapofika wakati wa uchaguzi
kila mmoja anatakiwa acheze mechi zake kutokana na nafasi walizo nazo.
Kitte amesema " Ukiwa Kiongozi
jipime kwa kutatua matatizo ya watu unaowaongoza ndipo uwezo wako utakupa tena
nafasi ya kuongozi."
Aidha amewataka viongozi hao kwenda katika maeneo yao na kuwaunganisha
Wanaccm ili kulinda umoja na heshima ya CCM.
Amemalizia kwa kuendelea kumpongeza Mhe, Daktari Samia Suluhu Hassan Mwenyekiti wa CCM Taifa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kutokana na kasi ya maendeleo anayoileta katika Taifa la Tanzania.
No comments