Breaking News

DIWANI MTANGA APITA NYUMBA KWA NYUMBA KUHAMASISHA KUJIANDIKISHA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA

Atembelea Kikundi cha Bwengo kuhamasisha Vijana kujiunga Vikundi kunufaika Mikopo ya asilimia kumi (10%).


Diwani wa Kata ya Ngamiani Kusini, kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Mtanga Aweso (kushoto), akiwa na wajumbe wa kamati yake kuhamasishaji Wananchi kujiandikisha kwenye Daftari la Kudumu la Wapiga kura.

................................

Na Mashaka Kibaya, Tanga.

WAKAZI wa Ngamiani Kusini Jijini Tanga,wametakiwa kuona umuhimu wa kujiandikisha kwenye daktari la kudumu la wapiga kura, ili kupata haki ya kuchagua Viongozi wao kwenye uchaguzi wa Serikali za Mitaa utakaofanyika Novemba 27 Mwaka huu.

Diwani wa Kata ya Ngamiani Kusini, Mtanga Aweso, Jana akiwa na Kamati yake kufanya uhamasishaji Wananchi kujiandikisha kwenye daftari la kudumu la wapiga kura, akisema kuwa uhamasishaji huo ni kupitia utaratibu wa  nyumba kwa nyumba.

Akiwa katika eneo la Mitaa ya barabara 17 Jijini Tanga, Diwani Mtanga alisema, tayari zoezi la uandikishaji limeanza, hivyo na wao kupitia nafasi zao wanao wajibu wa kuendelea kuwaelimisha wananchi umuhimu wa kujiandikisha kwenye daktari la kudumu.

Amesema kwamba, wananchi watakapochukua hatua ya kujiandikisha ndipo watakapopata fursa ya kuchagua Viongozi wao hatua ambayo itawasaidia katika kuharakisha maendeleo yao.

Licha ya Diwani Mwatanga kufanya hamasa juu ya Wananchi kujiandikisha kwenye daktari la kudumu la wapiga kura lakini pia alitumia fursa hiyo kuhamasisha Vijana kujiunga katika Vikundi ili kunufaika na mikopo ya Vijana, Wanawake na Walemavu.

Diwani huyo alisema kwamba, dirisha la utolewaji mikopo hiyo limeshafunguliwa na kuwa walengwa wanatakiwa kwenda kwenye Ofisi za Watendaji Kata ili kuweza kupewa miongozo juu ya namna wanavyoweza kunufaika na Mikopo hiyo.

"Kazi yangu ni kuelimisha wananchi, Serikali ya Rais Dkt Samia Suluhu Hassan imeanza kutoa mikopo...dirisha limeshafunguliwa hivyo vijana, wanawake na walemavu wajiunge katika vikundi ili kuweza kunufaika na mikopo ya asilimia kumi" alisema Diwani Mwatanga Aweso.

Katika ziara hiyo Diwani huyo aliambatana na Katibu wa Chama Cha Mapinduzi CCM Kata hiyo ya Ngamiani Kusini, Masika Mwinshehe, ambaye mbali na kuhamasisha zoezi la Wananchi kujiandikisha kwenye daktari la kudumu pia aliwakbusha wanaCCM kuwa na Kadi za  Kilelektroniksi.

"Ziara yetu hii lengo lake ni kuhamasisha wananchi kujiandikisha kwenye daktari la kudumu la wapiga kura, kama Chama pia tunatazama utekelezaji Ilani na kuhimiza uhai na ndio maana nakumbusha kadi za Kilelektroniksi"alisema Katibu CCM Kata,Masika Mwinshehe.

Aidha Masika amemshukuru Mbunge wa Jimbo la Tanga Mjini, Ummy Mwalimu, kwa kuwezesha upatikanaji wa Simu ya nyongeza ili kufanikisha utaratibu wa wanaCCM kuingia kwenye mfumo wa Kilelektroniksi.

Diwani wa Kata ya Ngamiani Kusini, Mtanga Aweso (katikati), akiwa na wajumbe wa kamati yake ya uhamasishaji watu kwenda kujiandikisha kwenye dafati hilo.
Diwani wa Kata ya Ngamiani Kusini, Mtanga Aweso (kushoto), na mmoja wa wajumbe wa kamati hiyo wakionesha furaha wakati wa zoezi la uhamasishaji.

No comments