Breaking News

RAIS SAMIA AZINDUA ZOEZI LA UANDIKISHAJI KATIKA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA

Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania hivi leo Tarehe 11.10.2024 Mkoani Dodoma amezindua zoezi la uandikishaji katika daftari la Mpiga kura na hapa yupo na wananchi wenzake wa Kitongoji cha Sokoine, Chamwino katika foleni ya kujiandikisha kwenye Daftari la Wapiga Kura kwa ajili ya Uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2024. 

Zoezi hili la siku 10 limeanza leo Tarehe 11 hadi 20 Octoba 2024. Tukumbuke Kauli Mbiu ya uchaguzi huu ni  Serikali za Mitaa ni Sauti ya Wananchi. Hivyo Rais Samia anawahimiza Watanzania wote wenye sifa za kuchagua na kuchaguliwa kujitokeza kwa wingi na kujiandikisha ili waweze kushiriki Uchaguzi huu muhimu Tarehe 27.11.2024.

 

No comments