Breaking News

DKT.MPANGO AWEKA JIWE LA MSINGI MRADI WA MAJI TABORA


Makapunwa Rais Dkt. Philip Mpango akiweka  jiwe la msingi la  mradi wa maji kutoka Ziwa Victoria kwenda katika miji ya Sikonge, Urambo na Kaliua wenye thamani ya shilingi Bilioni 143.26 iliyofanyika katika mji wa Sikonge Mkoani Tabora.

........................................

Na Mwandishi Wetu, Tabora 

MAKAMU wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango ametoa rai kwa wananchi kuhakikisha miundombinu ya  vyanzo vya maji  vinatunzwa ili idumu kwa muda mrefu.

Dkt.Mpango ametoa rai  hiyo kwenye Hafla ya uwekaji jiwe la msingi la  mradi wa maji kutoka Ziwa Victoria kwenda katika miji ya Sikonge, Urambo na Kaliua wenye thamani ya shilingi Bilioni 143.26 iliyofanyika katika mji wa Sikonge Mkoani Tabora.

Dkt.Mpango ameishukuru serikali ya India kwa ushirikiano mzuri ambao umewezesha kufanikisha maendeleo kwa serikali za Tanzania na India.

Awali akizungumzia mradi huo Naibu Waziri wa Maji Mhandisi Kundo Mathew (Mb) amesema mradi huo ni sehemu ya mradi wa maji wa miji 28 ambao unatekelezwa kupitia mkopo wenye masharti nafuu kutoka Serikali ya India.

Mhandisi Kundo  ameishukuru Serikali kwa kuendelea kutoa fedha kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya maji nchini.

Pia, Katibu Mkuu wa Wizara ya Maji Mhandisi Mwajuma Waziri amesema mradi huo ulianza kutekelezwa Aprili 2023 na utakamilika Oktoba 2025.

Mhandisi Mwajuma amemhakikishia Makamu wa Rais kuwa Wizara itaendelea kusimamia kuhakikisha mradi unakamilika kwa wakati.

Amesema mradi huo utazalisha lita miliomi 24.76 kwa siku na kuhudumia zaidi ya wakazi 490,926 waliopo katika miji ya Sikonge, Urambo, Kaliua na Uyui pamoja na vijiji 63 ambapo ameeleza kuwa  Ultekelezaji wa mradi huo umefika asilimia 48.

Taarifa ya mradi huo ikitolewa.
Taswira ya uzinduzi wa mradi huo.
Viongozi mbalimbali wakimsikiliza Dkt. Mpango (hayupo pichani)
Makamu wa Rais Dkt. Philip Mpango akipokea taarifa ya mradi huo. 

No comments