Breaking News

RC LINDI AWATAKA WANAWAKE KUWA NA MAAMUZI YASIYO LEGALEGA

Mkuu wa Mkoa wa Lindi, Zainab Telack

…………………………………

Na Mwandishi Wetu, Lindi

MKUU wa Mkoa wa Lindi, Zainab Telack ametoa wito kwa wanawake wa Mkoa wa Lindi kuwa na maamuzi na ujasiri Mkubwa katika kuyafikia malengo bila kugeuka nyuma.

Mhe. Telack ametoa wito huo katika hafla iliyoandaliwa na wome's Gala 2024 yenye lengo la kuwakutanisha wanawake wakada tofauti tofauti kubadilishana uzoefu na kupata elimu mbalimbali zitakazowezesha kuwaongezea maarifa katika nyanja za kiuchumi, kijamii , kiutamaduni na kisiasa.

"Sasa akina mama ili tuweze kufika huko, kufikia malengo ambayo tunataka kuyafikia , tunachotakiwa kuwa nacho ni ujasiri mkubwa , kuwa na maamuzi ambayo hayalegilegi kwenye yale ambayo unataka kwenda kuyafikia, usikatishwe tamaa na yoyote wakati unataka kwenda mbele kama lile unalofikiria unataka kwenda nalo unauhakika utatoboa na utafika unakotaka kwenda .

Amesema hatua hiyo ya kuchukua maamuzi yanatoka na changamoto nyingi ambazo mwanamke anakutana nazo.


 

No comments