Breaking News

TEA YASHIRIKI MAADHIMISHO YA KITAIFA YA JUMA LA ELIMU YA WATU WAZIMA TABORA, RAIS SAMIA ATAJWA

Mkuu wa  Kitengo cha Uhusiano na Mawasiliano kwa Umma wa Mamlaka ya Elimu Tanzania (TEA), Bi. Bestina Magutu akitoa maelezo kwa Wanafunzi na wadau mbalimbali waliotembelea banda la mamlaka hiyo kwenye  Maadhimisho ya Kitaifa ya Juma la Elimu ya Watu Wazima yanayoendelea katika Viwanja vya Chipukizi mkoani Tabora ambayo yameandaliwa na  Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

..............................

Na Mwandishi Wetu, Tabora

MAMLAKA ya Elimu Tanzania (TEA), ambayo ni Taasisi ya Serikali chini ya Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia imeshiriki Maadhimisho ya Kitaifa ya Juma la Elimu ya Watu Wazima yanayoendelea katika Viwanja vya Chipukizi mkoani Tabora .

Mkuu wa  Kitengo cha Uhusiano na Mawasiliano kwa Umma wa Mamlaka ya Elimu Tanzania (TEA), Bi. Bestina Magutu, akizungumza katika maadhimisho hayo   alisema maadhimisho hayo   yanatoa fursa nzuri kwa jamii kuelewa umuhimu wa elimu ya watu wazima na jinsi TEA inavyochangia katika maendeleo ya elimu nchini.

Alisema majukumu ya TEA kupitia mfuko wa elimu wa Taifa imekuwa ikiboresha mazingira bora ya kujifunzia na kufundishia na kuboresha miundombinu ya elimu kama madarasa na mingine yote.

Magutu alisema katika ushiriki wa maadhimisho hayo wamekutana na wadau mbalimbali na kuweza kubadilishana uzoefu wa namna ya kuongeza ufanisi wa uboreshaji wa miundombinu  ya elimu na namna ya kuitunza ikizingatiwa kuwa Serikali imekuwa ikitoa fedha nyingi kwa kazi hiyo.

“Maadhimisho haya   yanatoa fursa nzuri kwa jamii kuelewa umuhimu wa elimu ya watu wazima na jinsi TEA inavyochangia katika maendeleo ya elimu nchini na ndio maana tumeyahimiza makundi mbalimbali ya watu kuja kushiriki,” alisema  Magutu.

Alisema maadhimisho hayo   yanatoa fursa nzuri kwa jamii kuelewa umuhimu wa elimu ya watu wazima ambayo licha ya wahusika kuwa na umri mkubwa kupitia elimu hiyo imewaongezea maarifa na kupiga hatua kimaisha kwani baadhi yao walikuwa wamekatisha masomo yao kwa sababu mbalimbali. 

Katika maadhimisho hayo wanafunzi na wadau wengine mbalimbali wamekuwa wakifika banda la  mamlaka hiyo ili kuongeza uelewa juu ya utendaji kazi wake ambapo baadhi yao wamepongeza jitihada zinazofanywa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan za kuboresha miundombinu  ya elimu nchini.Afisa Miradi wa TEA, Lusungu Kaduma (kulia) akitoa maelezo kuhusu shughuli mbalimbali zinazofanywa na mamlaka hiyo kwenye maadhimisho hayo. Kutoka kushoto ni Bi. Eva Shumbusho  na katikati ni Afisa Utafutaji Rasilimali, Bi Joyce Minja.

Bi. Eva Shumbusho kutoka TEA, akitoa Elimu  kwa Umma kwenye maadhimisho hayo.
Elimu ikiendelea kutolewa kwenye maadhimisho hayo.

 Taswira ya maadhimisho hayo.

No comments