Breaking News

RAIS DKT.SAMIA ASISITIZA NCHI ZA SADC KUMALIZA MIGOGORO.


Rais wa Zanzibar Dkt. Hussein Ali .Mwinyi akihutubia kwa niaba ya Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan alipomwakilisha kufungua Mkutano wa  Viongozi Wakuu  na Serikali wa  Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika uliofanyika jijini Harare Zimbabwe Novemba 20,  2024.

.................................................

Na Mwandishi Wetu, Zimbabwe

Mwenyekiti wa asasi ya siasa, ulinzi na usalama wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC), Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Dkt.Samia Suluhu Hassan amezisisitiza  nchi za Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika SADC kuunga mkono juhudi za kidiplomasia za kumaliza Uhasama uliopo baina ya DRC na Rwanda chini ya mchakato wa Angola.

Rais wa Zanzibar Dkt. Hussein Ali .Mwinyi ameyasema hayo kwa niaba ya Rais Dkt.Samia alipomwakilisha kufungua Mkutano wa  Viongozi Wakuu  na Serikali wa  Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika uliofanyika jijini Harare Zimbabwe tarehe 20 Novemba 2024.

Rais Dk, Samia amefafanua kuwa wakati nchi za SADC zikiendelea kujadili hali ya  Usalama wa Mashariki ya  DRC ni vyema kukawekwa mifumo imara ya Ufuatiliaji na utekelezaji wa maazimio  yanayoidhinishwa na  Jumuiya mbalimbali za Kikanda ikiwemo  yale ya Umoja wa Afrika(AU) na Umoja wa Mataifa (UN).

Ameeleza kuwa hatua hiyo itawezesha kupatikana kwa Misaada ya kifedha na kilojistik  kwa wakati na kuongeza Ufanisi wa Misheni  za SADC na kupunguza gharama.

Rais Dk, Samia amezishauri nchi za SADC kutumia majadiliano ya Mkutano huo  kutoka na maazimio  yatakayokuwa chachu ya  kupatikana kwa Amani ya kudumu katika Ukanda wa SADC na kuwa ni ushahidi wa dhamira ya nchi hizo ya kuleta Amani Endelevu.Viongozi wakiwa kwenye mkutano huo.

Taswira ya mkutano huo.

Viongozi wakiwa katika picha ya pamoja
 

No comments