RC DENDEGO AZINDUA PROGRAMU ZA SHAHADA YA UZAMILI KATIKA MAHAFALI YA 22 TIA SINGIDA
Mkuu wa Mkoa wa Singida, Halima Dendego, akikata utepe
kuashiria uzinduzi wa Programu ya Shahada za Uzamili ilioanzishwa na
Taasisi ya Uhasibu Tanzania (TIA) wakati wa Mahafali ya 22 ya taasisi hiyo
Kampasi ya Singida yaliyofanyika Novemba 22, 2024. Kutoka kushoto wanaoshuhudia
tukio hilo ni Mjumbe wa Bodi ya Ushauri Wizara ya Fedha, Renatus Msangira, Mkuu
wa Wilaya ya Singida, Godwin Gondwe na Afisa Mtendaji Mkuu (CEO) wa TIA,
Prof. William Pallangyo.
Na
Mwandishi Wetu, Singida
MKUU wa
Mkoa wa Singida, Halima Dendego ameongoza uzinduzi wa Programu za Shahada ya Uzamili iliyoanzishwa na Taasisi ya Uhasibu Tanzania (TIA) Kampasi ya Singida.
Akizungumza
wakati wa uzinduzi huo, Dendego aliipongeza taasisi hiyo kwa kuanzisha programu
hiyo ambayo ni ya muhimu na akawaomba wana Singida na Wananchi wengine kuichangamkia na kueleza kuwa hiyo ni fursa kubwa kwao..
Ninayo furaha
kubwa kuwa Mgeni Rasmi katika Mahafali ya Ishirini na Mbili ya Taasisi ya
Uhasibu Tanzania, mahafali ambayo yanafanyika katika kampasi yetu ya Singida
kwa mara ya Kumi na Tatu.
"
Ninatoa shukurani zangu za dhati kwa Bodi ya Ushauri ya Wizara na Mtendaji
Mkuu wa Taasisi ya Uhasibu
Tanzania, kwa kunialika kushiriki na kuwa Mgeni Rasmi. Tangu
nilipowasili, nimepokelewa kwa heshima na ukarimu mkubwa, " alisema
Dendego.
Dendego
alipongeza kazi kubwa inayofanywa na taasisi hiyo, Bodi ya Ushauri, na
Uongozi wake wakiwemo watumishi kwa kusimamia vyema utekelezaji wa malengo ya
Taasisi kupitia Mpango Mkakati wake hususan katika utoaji wa mafunzo, tafiti,
na ushauri wa kitaalamu kwenye nyanja mbalimbali.
Aidha aliipongeza TIA kwa kufanyia kazi maelekezo ya Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,kwa kutoa elimu ujuzi inayowawezesha wanachuo
kujiajiri na kuzingatia kwa umakini suala la umahiri katika mitaala kwa lengo
la kupata wataalam wenye uwezo wa kuleta mabadiliko chanya ya kiuchumi.
Dendego alisema amevutiwa na juhudi za Mhadhiri Msaidizi wa taasisi hiyo
Mary Kayanda katika kuboresha somo la Hisabati shule za Singida na kueleza kuwa
huo ni mfano bora wa ubunifu na mchango wa Chuo hicho katika elimu na akatoa
mapendekezo mkakati huo uendelee na ujumuishwe na masomo mengine ya Biashara
kama Bookkeeping na Commerce, ili kuimarisha ujuzi wa wanafunzi.
"Nimesikia katika taarifa ya Mtendaji Mkuu Profesa Pallangyo kwamba watawatunuku wahitimu 1,477 hii ni faraja kubwa kwa Mkoa wetu wa Singida na Taasisi yetu ya Elimu hivyo nitoe wito kwa wahitimu kuwa, ingawa kuajiriwa ni fursa nzuri, kujiajiri ni bora zaidi, kwani inawapa nafasi ya kuwa wabunifu na uhuru wa kufikia malengo yenu, " alisema Dendego.
No comments