Breaking News

ZANZIBAR MPYA CHINI YA RAIS DKT. HUSSEIN ALI MWINYI YAWA NA MAPINDUZI MAKUBWA YA MAENDELEO

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt. Hussein Ali Mwinyi.  

............................

Na Dotto Mwaibale

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt. Hussein Ali Mwinyi ambaye ni Rais wa Nane wa Zanzibar amepeleka Neema nyingi kwa Wanzibar katika kipindi kifupi cha uongozi wake tangu aingie madarakani.

MAFANIKIO KADHAA YA SERIKALI YAKE KATIKA SEKTA YA UWEZESHAJI WANANCHI.

Tangu aingie madarakani Rais Dkt. Ali Hussein Mwinyi Serikali imeweza kutoa mikopo nafuu kwa wananchi 19,906 yenye thamani ya Sh. 22.5 Bilioni ikiwa ni ongezeko la Sh. 15 Bilioni zilizotolewa awali na kusababisha ajira kwa wananchi 43,360.

KATIKA ENEO LA ELIMU NA UJASIRIAMALI

 Serikali imeendelea kuendesha mifuko ya Khalifa na ule wa makundi 4.4.2 yaani Vijana asilimia 4, Wanawake asilimia 4 na Walemavu asilimia 2 kwa kutoa elimu ya ujasiriamali na mafunzo ya utaalamu wa biashara pamoja na kuwaunganisha na masoko.

VYAMA 3,666 VIMESAJILIWA

Katika awamu yake hii ya uongozi vyama vya ushirika 3,666 vimesajiliwa vikiendesha shughuli na mitaji. Vyama Mwamvuli vitatu vya maziwa, uvuvi na ushoni vimeimarishwa kwa mafunzo, mitaji na ufuatiliaji wa madeni.

No comments