KANISA LAMPA TUZO MBUNGE JIMBO LA BUSOKELO KUTAMBUA MAENDELEO YALIYOFANYIKA
...............................................
Na Mwandishi Wetu, Rungwe
Katika Ibada ya Mwaka Mpya Iliyofanyika Katika Kanisa la Tanzania
Assemblies of God JCC Lwangwa imetambua kazi zinazofanywa na Mbunge wa Jimbo la
Busokelo Atupele Fredy Mwakibete na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania Dkt.Samia Suluhu Hassan.
Ibada hiyo iliyoongozwa na Mchungaji Kelvin Kwileka imefanya maombi maalum
kwa viongozi akiwemo Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, Makamu wa Rais
Dkt. Phillip Isdor Mpango, Waziri Mkuu Kassim Majaliwa pamoja na Mbunge wa
Jimbo la Busokelo Atupele Fredy Mwakibete, kisha kukabidhi tuzo kama ishara ya
kutambua kazi iliyotukuka na inayoonekana jimboni inayofanywa na viongozi hao.
Aidha, Katika Ibada Hiyo Mheshimiwa Mwakibete amelishukuru Kanisa kwa
maombi hayo pamoja na tuzo ya kutambua kazi inayofanywa na serikali ya awamu ya
sita,pia ameweza kuchangia ujenzi wa ofisi ya mchungaji unaondelea kwa pesa
Taslimu Shilingi Milioni Moja na Tripu Tano za Mchanga.
No comments