Breaking News

RAIS MWINYI: SERIKALI ITAENDELEA KUJENGA NYUMBA ZA KISASA ZA WANANCHI

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi akihutubia wakati wa  Ufunguzi wa Nyumba 72 za Makaazi na Biashara  Mombasa kwa  Mchina  Wilaya ya Magharibi B Mkoa wa Mjini Magharibi zilizojengwa na Shirika la Nyumba la Zanzibar.

.................................................

Na Mwandishi Wetu, Zanzibar 

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi amewathibitishia Wananchi kuwa Serikali itaendelea Kujenga Nyumba za Kisasa Maeneo  yote ambayo yana Nyumba zilizo Chakavu kwa lengo la kuwapatia Wananchi Makaazi bora.

Rais Dk. Mwinyi ameyasema hayo katika Ufunguzi wa Nyumba 72 za Makaazi na Biashara  Mombasa kwa  Mchina  Wilaya ya Magharibi B Mkoa wa Mjini Magharibi zilizojengwa na Shirika la Nyumba la Zanzibar.

Rais Dk.Mwinyi ameiagiza Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makaazi  kuandaa Mpango Maalum wa  Kisheria wa Matunzo ya Nyumba  inazozijenga ili Suala la Matunzo kuwa la Lazima na Sio hiyari.

Rais Dk. Mwinyi  amefahamisha kuwa  Mpango huo ni lazima Uzingatie Mifumo ya Maji, Masuala ya Usafi na Uangalizi wa Nyumba zenyewe Ili ziendelee kuwa na Haiba  nzuri ilizonazo hivi sasa.

Aidha, Rais Dk. Mwinyi  amewashauri Wamiliki wa Nyumba hizo kuanzisha Kamati Maalum za  Matunzo ya Nyumba hizo  kwa kila Mmiliki kuwajibika na Usafi na Matunzo  ya Nyumba anayomiliki.

Rais  Dk.Mwinyi  amesisitiza kuwa  Wananchi ni lazima   Wakubali kupisha Miradi ya  Ujenzi wa Nyumba  na kwamba Serikali itawafidia  Nyumba Bora za Makaazi  badala ya Fedha .

Halikadhalika Rais Dk. Mwinyi ameeleza kuwa  Wananchi Kukaa katika Makaazi mazuri ndio dhamira ya Serikali  na kuwa Mpango wa Ujenzi wa Nyumba 3000 eneo la Chumbuni   utaendelea katika maeneo  mengine  na kuwaambia Wakaazi wa Kikwajuni kukaa tayari kwani nyumba mia tano zitajengwa  katika eneo hilo na  Serikali ipo tayari kwa Mradi huo.

Rais Dk. Mwinyi ameeleza kuridhika na Utendaji wa Wizara hiyo  kwa Mafanikio Makubwa ya Miradi ya Ujenzi wa Nyumba.

No comments