KAMPUNI ZA EMIRATES LEISURE NA DNATA ZATOA MSAADA KWA KITUO CHA WAHITAJI ZANZIBAR
Wafanya kazi wa Kampuni za za Emirates Leisure na DNATA Zanzibar wakiwa katika picha ya pamoja na watoto wenye uhitaji wa Kituo cha Markaz Lyaqiin Islamic Center kilichopo Kinduni Zanzibar baada ya kuwapatia msaada wa vitu mbalimbali.
.........................................
Na Mwandishi Wetu, Zanzibar
KAMPUNI za
Emirates Leisure na DNATA Zanzibar zimetoa msaada wa vitu mbalimbali katika Kituo
cha Watoto Yatima cha Markaz Lyaqiin Islamic Center kilichopo Kinduni Zanzibar.
Akizungumza
katika hafla ya kukabidhi msaada huo, Meneja Mkazi wa Kampuni ya Emirates
Leisure, Mr Paul Attallah alisema utoaji wa msaada huo ni mwendelezo wa kampuni
hizo katika kuungamkono jitihada za Serikali ya Mapinduzi Zanzibar chini ya
Rais Dkt. Hussein Ali Mwinyi za kuwajali wanananchi.
“ Msaada huu
tunao utoa ni mwendelezo wa ratiba yetu ya kuwashika mkono watu wenye uhitaji na pia
kuunga mkono jitihada za Serikali ya Rais wa Zanzibar Dkt. Hussein Ali Mwinyi
ambaye siku zote amekuwa akizitaka kampuni mbalimbali kuwa na utamaduni wa kurudisha
kwa jamii faida wanayoipata kwa kuyasaidia makundi maalumu yenye uhitaji kwa
lengo la kuwapa furaha, “ alisema Attallah.
Kwa upande
wake Afisa Utawala wa Kampuni ya Emirates
Leisure, Msokolo Layya alisisitiza
kudumisha ushirikiano baina ya kampuni hizo na kueleza kuwa wataendelea
kusimamia ratiba ya kutoa msaada kwa wahitaji katika kipindi cha mwaka mzima
kama walivyopanga.
Katika hafla
hiyo viongozi mbalimbali wa kampuni hizo walikuwepo wakiongozwa na Meneja Mkazi
wa Kampuni ya Emirates Leisure, Paul Attallah,
Mkuu wa Fedha wa kampuni hiyo, Noah
Mwansa, Shuwea, Commacial Support wa DNATA, Kaimu Rasilimali
Watu na Utawala wa Kampuni ya DNATA, Bi. Lucy na Afisa Utawala wa Emirates
Leisure, Msokolo Layya.
Wengine
wliohudhuri hafla hiyo ni wawakilishi toka kampuni hizo, Meneja Usafirishaji wa
Kampuni ya DNATA, Anthony, Meneja wa Kampuni ya DNATA na Compliance Manager wa
Kampuni ya DNATA, Mr George na Bi Zainab kutoka Kampuni ya DNATA.
Viongozi wa wa
kituo hicho wamezishukuru kampuni hizo kwa msaada mkubwa walioutoa kwa ajili ya
watoto hao wenye uhitaji.
Msaada huo ukikabidhiwa.
Msaada ukikabidhiwa kwa walengwa

No comments