Breaking News

MBUNGE SUMA FYANDOMO ATOA SALAMU ZA SHUKURANI KWA WASIRA, AWATAKA WANA CCM MBEYA KUSHIKAMANA


Mbunge wa Viti Maalumu Mkoa wa Mbeya, Suma Fyandomo akizungumza wakati akitoa Salamu za shukurani baada ya kumalizika kwa ziara ya Makamu Mwenyekiti wa CCM Tanzania Bara, Ndugu Stephen Wasira aliyoifanya Mkoa wa Mbeya.

...........................................

Na Mwandishi Wetu, Mbeya

MBUNGE wa Viti Maalum Mkoa wa Mbeya. Suma Fyandomo ametoa Salamu za shukurani baada ya kumalizika kwa ziara ya Makamu Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Tanzania Bara, Ndugu Stephen Wasira aliyoifanya Mkoa wa Mbeya hivi karibuni.

Aidha, Mbunge Fyandomo ameushukuru uongozi wa CCM Mkoa wa Mbeya, wanachama wa CCM na wananchi kwa ushirikiano wao katika kufanikisha ziara hiyo muhimu kwa chama na Taifa kwa kuzingatia kuwa chama hicho ndicho kimeshika dola.

Fyandomo alitumia nafasi hiyo kupongeza hotuba ya makamu mwenyekiti huyo wa CCM Tanzania Bara aliyotoa wakati wa ziara zake ndani ya Wilaya za Mkoa wa Mbeya na kueleza  kuwa imeleta msukumo mpya wa maendeleo ya mkoani humo na kuwa maagizo aliyowapa watayatekeleza.

Hata hivyo, Fyandomo amewahimiza wana CCM mkoani Mbeya kuendelea kushikamana na kutekeleza Ilani ya CCM kwa vitendo ili kuimarisha maendeleo ya jamii na kuhakikisha chama hicho kinapata ushindi katika uchaguzi mkuu utakaofanyika Oktoba mwaka huu.

Mbunge Fyandomo baada ya kutoa salamu hizo aliongoza zoezi la ugawaji zawadi kwa Makamu Mwenyekiti wa CCM Tanzania Bara, Ndugu Stephen Wasira ambaye amehitimisha ziara yake mkoani humo na kuanza ziara ya kikazi mkoani Kagera.

Mbunge wa Viti Maalumu Mkoa wa Mbeya, Suma Fyandomo akiongoza shamra shamra wakati wa ziara hiyo ya Makamu Mwenyekiti wa CCM Taifa, Stephen Wasira mkoani humo.

Mbunge wa Viti Maalumu Mkoa wa Mbeya, Suma Fyandomo (kushoto) akiongoza akiongoza utoaji wa zawadi kwa Makamu Mwenyekiti wa CCM Taifa Tanzania Bara, Ndugu Stephen Wasira.
Zawadi kwa Makamu Mwenyekiti wa CCM Taifa Tanzania Bara, Ndugu Stephen Wasira zikitolewa..
Makamu Mwenyekiti CCM Tanzania Bara Ndugu Stephen Wasira akipokea zawadi.
 

No comments