MSAMA AWATAKA VIONGOZI WA DINI KUTOJIHUSISHA NA SIASA KWENYE NYUMBA ZA IBADA
Mkurugenzi wa Msama Promotions, Alex Msama, akizungumza na waandishi wa habari Juni 8, 2025 Jijini Dar es Salaam na kueleza kusikitishwa kwake na baadhi ya viongozi wa dini ambao wanatumia nyumba za ibada kufanya siasa.
...............................................
Na Mwandishi Wetu
VIONGOZI wa dini wametakiwa
kuacha kutumia nyumba za ibada kufanya siasa na kuwa kazi hiyo waachie wana
siasa wenyewe.
Ombi hilo limetolewa na Mkurugenzi
wa Msama Promotions Alex Msama wakati akizungumza na waandishi wa habari Jijini
Dar es Salaam na kueleza kusikitishwa kwake na baadhi ya viongozi wa dini ambao
wamekuwa wakifanya hivyo.
“Vyombo vya dola vichukue
hatua kali dhidi ya viongozi wa dini ambao wanatumia makanisa na misikiti kuzungumzia
masuala ya siasa badala ya kuhubiri neon la Mungu,” alisema Msama.
Msama akizungumza katika
mkutano huo huku akinukuu baadhi ya vifungu kutoka katika biblia Takatifu kitabu
cha warumi aliwataka viongozi hao kuheshimu mamlaka zilizowekwa na Mungu na
kueleza kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan yupo
katika nafasi hiyo baada ya kuwekwa na Mungu hivyo kumdhihaki na kumtukana ni
kukinzana na Mungu.
“Kitabu cha warumi 13
mstari wa pili kinaeleza kuwa amuasie mwenye mamlaka anashindana na agizo la Mungu
hivyo mambo ya siasa waachiwe wanasiasa kwani mtu hawezi kuwatumikia mabwana
wawili lazima atampenda mmoja na mwingine atamchukia,” alisema Msama,
Aliongeza kuwa kila kiongozi wa dini anayechanganya dini na siasa
anachokitafuta ndicho atakivuna hivyo anapokutana na mkono wa dola asilalamike
wala kumtupia mtu lawama badala yake atubu na kumuomba msamaha Rais ambapo
aliwaomba wafanye kazi ya Mungu na wasiingiwe na roho za tamaa za kishetani.
“Kafanyeni kazi ya kuwavuta watu kutoka kwa shetani na
kuwaleta kwa Mungu kwa kuyacha matendo yote maovu yakiwemo ya kuvuta bange,”
alisema Msama.
Mkurugenzi wa Msama Promotions Alex Msama akisisitiza jambo kwenye mkutano huo.
Post Comment
No comments