Breaking News

MAPURI: KASIMAMIENI MAFUNZO MLIYOFUNDISHWA KWA KUZINGATIA, KATIBA, SHERIA NA KANUNI

Mjumbe wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) Balozi Omar Ramadhan Mapuri akifunga mafunzo ya siku tatu kwa waratibu wa uchaguzi, wasimamizi na maafisa kutoka mikoa ya Dar es Salaam na Pwani yalioanza Julai 21, 2025 na kufikia tamati leo Julai 23, 2025 Jijini Dar es Salaam.

....................................................

Na Dotto Mwaibale, Dar es Salaam

WARATIBU wa uchaguzi, wasimamizi na maafisa kutoka mikoa ya Dar es Salaam na Pwani wametakiwa   kwenda kusimamia mafunzo waliyofundishwa kwa kuzingatia Katiba, Sheria na Kanuni.

Hayo yamesemwa na Mjumbe wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) Balozi Omar Ramadhan Mapuri wakati akifunga mafunzo ya siku tatu kwa waratibu wa uchaguzi, wasimamizi na maafisa kutoka mikoa hiyo yaliyofikia tamati leo Julai 23, 2025 Jijini Dar es Salaam.

Kasimamieni mafunzo mliyofundishwa kwa kuzingatia Katiba, sheria na Kanuni na si vinginevyo,” alisema Mapuri.

Aliwataka washiriki wa mafunzo hayo kwenda kuyatoa kwa wasimamizi Wasaidizi wa Uchaguzi ngazi ya Kata na watendaji wa vituo vya kupiga kura kwa weledi wa hali ya juu.

Aidha,Mapuri aliwataka washiriki hao kwenda kusimamia rasilimali na vifaa watakavyopewa na Tume kwa ajili ya  utekelezaji wa kazi za uchaguzi na kuvihakiki vifaa hivyo  mara tu watakapovipokea na kutoa taarifa haraka kwa Tume iwapo kutakuwa na  upungufu.

Katika hatua nyingine Mapuri aliwataka washiriki hao wa mafunzo hayo kwenda kusimamia  vyema matumizi ya fedha watakazotumiwa kwa ajili ya shughuli za uchaguzi.

” Kura yako haki yako jitokeze kupiga kura” 

Mwenyekiti wa mafunzo hayo, Selemani Kateti, akizungumza wakati akimkaribisha mgeni rasmi Balozi Ramadhani Mapuri kufunga mafunzo hayo.
Mjumbe wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) Balozi Omar Ramadhan Mapuri akiwa na Mratibu wa Uchaguzi Mkoa wa Dar es Salaam, Gelard Sondo.
Afisa wa Tume Huru ya Uchaguzi (INEC), Johari Mutani akizungumza wakati wa kufunga mafunzo hayo.
Washiriki wa mafunzo hayo wakiandika maelezo yaliyokuwa yakitolewa na Balozi Ramadhani Mapuri.
Washiriki wa mafunzo wakiwa kwenye mafunzo hayo
Mafunzo yakifungwa.
Mafunzo yakifungwa.
Taswira ya mafunzo hayo.
Washiriki wa mafunzo hayo wakiwajibika ipasavyo.
 

No comments