DKT. ASHA- ROSE MIGIRO MWANAMKE WA KWANZA KUWA KATIBU MKUU CCM
................................................
Na Dotto Mwaibale, Dar es Salaam
Dkt. Asha-Rose Migiro ni mwanamke wa kwanza kuwa Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), nafasi ambayo haijawahiu kushikwa na mwanamke yeyote tangu Tanzania ipate uhuru wake mwaka 1961.
Nafasi hiyo ya Dkt. Migiro imekuja
kufuatia uteuzi uliofanywa na Kikao cha
Halmashuri Kuu ya CCM (Taifa) chini ya Mwenyekiti wake na Rais wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania Dkt.Samia Suluhu Hassan.
Dkt. Migiro anashika nafasi
hiyo ya juu katika chama hicho akimrithi Dkt. Emmanuel Nchimbi ambaye
aliteuliwa kuwa mgombea mwenza wa Dkt. Samia wa nafasi ya urais kupitia chama
hicho.
Pamoja na kuteuliwa kuwa Katibu Mkuu wa CCM,Dkt. Migiro ana historia
ya kipekee pia nchini kwani ni mwanamke wa kwanza kuwa Naibu Katibu Mkuu wa
Umoja wa Mataifa chini ya Katibu Mkuu wa umoja huo aliyestaafu Ban Ki-moon.
Kikao hicho pia kilimteua aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Arusha Kenani Kihongosi kuwa Katibu wa NEC Itikadi, Uenezi na
Mafunzo wa chama hicho Taifa, akichukua nafasi ya Amos Makalla ambaye
ameteuliwa kuwa Mkuu wa Mkoa wa Arusha.
Dkt.Migiro alizaliwa mwaka 1956 na aliwahi kuwa Naibu Katibu Mkuu
wa Umoja wa Mataifa. Alipewa cheo hicho na Katibu Mkuu wake Ban
Ki-moon Januari 5, 2007
Hadi
kuteuliwa kwa cheo cha Umoja wa Mataifa alikuwa Waziri wa Mambo
ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa wa Tanzania tangu Januari 2006.
Nafasi
hiyo alipewa na Rais Jakaya Kikwete aliyemteua kumfuata
katika Wizara ya Mambo ya nje iliyoshikwa awali na Kikwete mwenyewe.
Chini
ya Rais Benjamin Mkapa Migiro alikuwa Waziri wa Maendeleo ya
Jamii, Jinsia na Watoto. Alikuwa Mbunge wa viti maalumu wanawake.
Kabla
ya kujiunga na siasa alifundisha kwenye Chuo Kikuu cha Dar es
Salaam. Alisoma Shahada ya Awali na Shahada ya Uzamili katika
chuo hichohicho.
Mwaka 1992 akaongeza Shahada
ya Udaktari wa Sheria kwenye Chuo Kikuu cha Konstanz
(Ujerumani). Akarudi Tanzania na kuanza kufundisha.
Dkt, Asha alifunga ndoa na Cleophas Migiro na kujaaliwa kupata watoto wawili wa kike.
Katibu wa NEC Itikadi, Uenezi na Mafunzo CCM Taifa, Kenani Kihongosi
No comments