Breaking News

SIKU NNE ZA MATESO WODINI MZEE HUYU, ANAOMBA MSAADA WA MATIBABU

Ana miaka 68, amekwisha katwa kidole, yupo Temeke Hospitali hajui hatima yake

Anachangamoto ya kutosikia, zinatakiwa Sh.220, 000 ili afanyiwe kipimo cha CT-SCAN. 

Mahitaji mengine ya kibinadamu ni changamoto.

Wasamaria wema wanaomsaidia waomba msaada zaidi wa watanzania.

Mzee Said Bakari Nyumbu (68), akiwa nyumba anayoishi.

............................................

Na Dotto Mwaibale, Dar es Salaam

 Mzee Said Bakari Nyumbu (68) Mkazi wa Mtaa wa Ngurungu , Maji Matitu (A) Mbagala Jijini Dar es Salaam maisha yake yako hatarini kufuatia maradhi yanayomsibu na sasa anaomba msaada wa Sh. 220,000 ili afanyiwe kipimo cha CT-SCAN aendelee na matibabu.

Mzee huyo ana siku ya nne sasa  amelazwa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Temeke kwa matibabu lakini yupo katika wakati mgumu kutokana na kutokuwa na uwezo wa kifedha zaidi ya kuwategemea wasamaria wema ambao wamelazimika kuwaomba watanzania kujitokeza kumsaidia mzee huyo ili kuokoa maisha yake.

Mzee huyo anachangamoto ya kutosia, amekatwa kidole cha mguuni lakini kutokana na kuathirika zaidi mguu wake madaktari wamemuambia anatakiwa afanyiwe kipimo cha CT-SCAN kuanzia kiuoni hadi miguuni ili kuona kama atakuwa ameathirika zaidi baada ya kujichoma na kitu chenye ncha kali katika kidole kilichokatwa alipokuwa kwenye miangaiko yake ya kujitafutia riziki.

Hali ya mzee huyo siyo nzuri kutokana na maisha duni aliyonayo na maradhi yanamsumbua.

Mbali ya kukatwa mguu pia anatakiwa kufanyiwa upasuaji wa tezi dume lakini ameshindwa kufanyiwa baada ya kukosa Sh. 700,000 za kufanyiwa upasuaji.

Ndugu watanzania hizo ndiyo shida anazopitia mzee wetu huyu, anaomba msaada wa hali na mali ili aweze kupata fedha za kumsaidia kupata matibabu na fedha za kujikimu.

Kama utaguswa kumsaidia unaweza kuwasiliana na Mzee Ally Abdallah Ngurungu na pia  Mjumbe wa Shina namba Nne Mwajuma Mshana ambao wanamsaidia kwa namba ya simu 0784679755 (Ally Abdallah Ngurungu) au Mwandishi wa Taarifa hii kwa namba 0754362990 kwa maelezo zaidi.

Ndugu Watanzania kwa kiasi chochote cha fedha utakacho jaaliwa na Mwenyezi Mungu iwe Sh. 1000, 2000, 5000 na zaidi ya hapo ukitoa zitamsaidia mzee huyu ambaye hajui hatima ya maisha yake na jambo kubwa zipatikane fedha za kipimo hicho cha CT-SCAN zinazohitajika. Kutoa ni moyo na Mungu atakubariki kwa utoaji wako.

Shime watanzania kwa umoja wetu tushikamane kumsaidia mzee wetu Saidi Nyumbu kuokoa maisha yake.

Changamoto ya ugonjwa ya Mzee Saidi Nyumbu imeibuliwa na Wajumbe wa Serikali ya Mtaa wa Matitu A kupitia CCM, ikiwa ni moja ya njia ya kutatua changamoto za wananchi wajumbe hao ni Hawa Omari na Jihadi Umwagala. 

Mzee Said Bakari Nyumbu (68) akiwa na Mzee Ally Abdallah Ngurungu (kushoto), ambaye wamekuwa wakimsaidia na wasamaria wema.
 

No comments