ANGELO MADUNDO ANAVYOING’ARISHA JUMUIYA YA WAZAZI CCM MBINGA
Ajivunia mambo matatu
Awaomba wananchi na wana CCM kujitokeza kwa wingi kumlaki Dkt. Samia ambaye atawasili Septemba 21, 2025 Mkoa wa Ruvuma.
Mratibu wa timu ya kampeni za Mgombea Ubunge Jimbo la Mbinga Vijijini Angelo Madundo, akimnadi Mgombea huyo Wakili Judith Kapinga kwenye moja ya mikutano ya kampeni inayoendelea kwa kasi jimboni humo.
.................................
Na Dotto Mwaibale
Jumuiya wazazi wa CCM ndiyo
jumuiya mama kati ya jumuiya zote kwa maana nyingine tunaweza kusema ndiyo
injini ya chama.
Viongozi wa Jumuiya hiyo kuanzia
Mwenyekiti wake, Katibu Mkuu wa Taifa, Mkoa, Wilaya hadi kata tumeona namna ambavyo wamekuwa
wakishirikiana na jumuiya nyingine za chama hicho katika kutekeleza majukumu ya
kazi ya kila siku.
Katibu Mkuu wa Jumuiya hiyo
Taifa, Ally Hapi tumekuwa tukimuona jinsi ambavyo hapati hata muda wa kupumzika
ili kuhakikisha shughuli mbalimbali ndani ya jumuiya hiyo zinakwenda sawa.
Hali hiyo imekuwa ikiigwa na
watendaji wa jumuiya hiyo nchini jambo
ambalo ni zuri katika ustawi wa CCM kupitia jumuiya zake zote.
Jumuiya hizo ni Umoja wa
Wanawake Tanzania (UWT), Umoja wa Vijana wa CCM (UVCCM), Seneti ya Vyuo na Vyuo
Vikuu na idara ya Chipukizi ambayo inaanzia chini kabisa kuwaandaa watoto
katika malezi na maadili.
Nimeanza kuandika Makala hii
kwa kuelezea majukumu na umuhimu wa Jumuiya hii ya wazazi ni kutokana na
kuwapika viongozi wake katika utekelezaji wa majukumu yake, leo napenda
kumzungumzia Angelo Madundo ambaye ni Katibu wa Jumuiya hiyo Wilaya ya Mbinga
mkoani Ruvuma.
Madundo amekuwa akifanya kazi
zake bila ya kuchoka wakati wowote unapompigia simu kwa ajili ya kazi simu yake
inapokelewa kwa wakati na kukusikiliza.
Jambo hilo linaleta matumaini
kwa wananchi ambao wanahitaji kupata huduma mbalimbali kupitia kwa viongozi wa
jumuiya kubwa kama hiyo ndani ya CCM.
Madundo tumemuona jinsi ambavyo
anashirikiana na jumuiya za chama hicho na viongozi wa chama hicho katika wilaya
hiyo wakati wa utekelezaji wa majukumu yake ya kazi jambo ambalo linaleta afya ya maendeleo
katika wilaya hiyo.
Hatua hiyo, inaonesha
mshikamano wa dhati ambao unaunga mkono moja kwa moja jitihada za Rais Dkt.
Samia Suluhu Hassan za kuwaletea wananchi maendeleo kutokana na uwajibikaji
wenye tija kwa taifa.
Hivi sasa Taifa letu lipo
kwenye kampeni za uchaguzi mkuu utakaofanyika oktoba 29, 2025 ambapo
tutamchagua rais, wabunge na madiwani ambapo chama kitakachopata ushindi
kitaingia kushika dola.
Kwa Jimbo la Mbinga Vijijini
ambalo mgombea nafasi ya ubunge kupitia CCM ni Wakili Judith Kapinga (Maarufu
kama Malikia wa Mbinga), wao wameunda kamati maalum ya ushindi huku Madundo
akiwa ni Mratibu wa timu ya kampeni na Mwenyekiti wa kampeni hizo akiwa ni John Bosco Mkandawile.
Kupitia kamati hiyo tumeona
kasi ya kampeni zinazofanyika katika jimbo ambapo kwa siku moja wanafanya
kampeni katika kata zaidi ya tatu na vijiji sita huku mikutano yao ikijaza watu
kutokana na kuiandaa vizuri.
Katika mikutano hiyo tumeona
jinsi mgombea nafasi ya ubunge anavyo tangaza sera na kuinadi ilani ya chama
hicho na kumuombea kura mgombea wa urais, diwani na yeye mwenyewe huku akihimiza
oktoba 29 wajitokeze kwa wingi kwenda kupiga kura na kuwachagua viongozi
wanaotokana na CCM.
Katika maeneo mengine ya
mikutano hiyo viongozi wa kamati hiyo wamekuwa wakimnadi mgombea huyo wa nafasi
ya ubunge na kumuombea kura rais, mbunge na diwani wa kata husika.
Madundo anasema kujiandisha
kwenye daftari la kudumu la mpiga kura ni jambo moja lakini jambo ambalo ni
kubwa na la msingi ni siku ya kupiga kula wananchi wote na wana CCM wajitokeze
kwenda kupiga kura
Ushirikiano wa namna hiyo
unaonesha mafanikio ya mapema ya ushindi wa chama hicho kutokana na jinsi
walivyojipanga.
Madundo anasema tangu aanze
kufanya kazi katika wilaya hiyo zaidi ya miaka mitano anajivunia mambo makubwa
matatu la kwanza likiwa ni kuifufua Shule ya Sekondari ya Mkinga ambayo ni ya Jumuiya ya Wazazi
ambayo aliikuta ipo taabani.
Aliongeza kuwa utokana na hali hiyo
alitoa taarifa makao makuu ambao walimpa baraka zote za kuinusuru shule hiyo
ili ili irudi katika hali yake ya kawaida.
Madundo anasema shule hiyo
aliikuta ikiwa na wanafunzi 120 haina jengo la utawala, madarasa machache ambapo alitengeneza mpango kwa ajili ya kuwapata wadau wa maendeleo ili
kusaidia jambo hilo.
Anasema wadau wa kwanza
walikuwa ni viongozi wa chama na Serikali ambao kwa umoja wao walifanikisha
kujenga jengo kubwa la kisasa la utawala.
Anasema kazi nyingine
aliyoifanya katika shule hiyo alianzisha kidato cha tano na cha sita kwa lengo
la kuongeza idadi ya wanafunzi na huduma ya masomo ya juu kwa wanafunzi hao
hatua ambayo imeongeza wanafunzi kutoka 120 mwaka 2020 hadi kufikia zaidi ya 351.
“ Katika rekodi za kitaaluma
shule yetu imekuwa ya kwanza kwa kuongoza matokeo kiwilaya lakini kimkoa mara
kwa mara imekuwa ishishika nafasi ya kumi bora,” alisema Madundo.
Anasema katika eneo hilo la
elimu anashukuru Mungu na Serikali kwani wamepiga hatua nzuri na wanatarajia
kufanya vizuri zaidi siku za mbele kutokana na ushirikiano mkubwa uliopo baina
yao na wadau wa maendeleo.
Madundo anasema jambo la pili ambalo
anajivunia ni ujenzi wa nyumba ya Katibu wa Jumuiya ya Wazazi ya Wilaya ambayo
ipo Mbinga Mjini na kazi hiyo ilifanikiwa baada ya kuwashirikisha wadau
mbalimbali wa maendeleo.
“Kutokana na kazi hizo kikao
cha kamati ya utekelezaji Mkoa wa Ruvuma kilinitunuku barua ya kunipongeza
jambo ambalo nashukuru sana,” alisema Madundo.
Anasema mafanikio ya tatu
ameanzisha mradi wa duka la kisasa la makaa yam awe ambao upo katika hatua za
majaribio na jingo lake limekwisha kamilika.
Anasema isingekuwa suala la
uchaguzi wangekuwa wameuzindua chini ya kauli mbiu yao ya ‘Uchumi na Siasa’
aliyoianzisha.
Madundo anasema kuwa lengo la kuanzisha
mradi huo ni kulenga viongozi wa kisiasa kupitia jumuiya zao kuhamasika kuwa na
miradi ya kuwaongezea kipato.
Anasema kupitia mradi huo
wameingia ubia na Kampuni ya Jitegemee ambayo ni ya CCM kwa ajili ya kuchukua
bidhaa ya kupikia na kuisambaza kwenye shule mbalimbali, mahotelini na maeneo
mengine yanayotumia nishati hiyo kwa matumizi ya kupikia.
Anasema kwa wakala waliopewa
watakuwa wasambaji wakuu wa nishati hiyo kwa mkoa mzima wa Ruvuma.
“Nshukuru kwa kipindi hiki
ambacho nikiwa kama kiongozi, jumiya yetu imebadilika ndani ya Wilaya ya Mbinga
na mkoa kwa ujumla kwa kuitambulisha kwa mambo tofauti kwenye maeneo ya ziara
za kimkakati za kuimarisha chama,” alisema Madundo.
Madundo anasema ushirikiano
mkubwa na jumuiya za chama hicho na idara za Serikali mkoani hapo ndiyo siri
kubwa ya mafanikiyo yao.
Akizungumzia kuhusu mchakato wa
uchaguzi mkuu anasema malengo ya Jimbo la Mbinga Vijijini ni kuongoza kwa kra
za rais kitaifa na kwa takwimu za kwetu mgombea wetu wa nafasi ya ubunge Judith
Kapinga aliongoza kwa kupata kura nyingi zaidi ya 12,000 kitaifa za kura za
maoni.
“Malengo yetu ni kuongoza
kitaifa kwa kura zote kuanzia za rais, mbunge na madiwani,” aliseam madundo.
Madundo aliongeza kuwa mikutano
yao yote wanayoifanya imekuwa na mafanikio makubwa kwani chini yake imeratibiwa
vizuri kisayansi na ina jaza watu.
Alisema hali hiyo ni ishara tosha ya kupata kura nyingi kutokana na wananchi kukielewa chama na sera zake na zaidi wagombea wao ni wazuri kuanzia rais, mbunge na madiwani hivyo wanarajia kuwa ndani ya majimbo matano bora nchi nzima yakatakayofanya vizuri kwa kupata kura nyingi.
Aidha, Madundo alitumia nafasi hiyo kuwaomba wana Mbinga kujitokeza kwa wingi kumpokea Mgombea wa nafasi ya Urais wa CCM Dkt. Samia Suluhu Hassan ambaye anatarajia kuwasili mkoani Ruvuma siku ya Jumapili Septemba 21, 2025.
No comments