Breaking News

KHAMBAY MBUNGE MWENYE SHUKURANI, MAONO

 Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wilaya ya Babati Mjini, Elezabeth Malley, akisalimiana na Mbunge wa Jimbo la Babati Mjini Mhe. Emmanuel Khambay,alipowasili kwenye kikao maalum cha Halmashauri Kuu ya CCM, wilayani humo Januari 4, 2026.

...................... 

Na Dotto Mwaibale

Uongozi ni mamlaka ya kuwaonyesha watu njia kwa vitendo ni dhana au taaluma inayompa mhusika madaraka na uwezo wa kuwawezesha wale wanaongozwa naye kuunganisha nguvu na vipaji vyao na kuvitumia ili kufikia malengo ya maendeleo.

Bora kiongozi ni kiongozi ambaye anafanya kazi bila ya kushirikiana na wananchi  anachoamua ndicho anataka kifuatwe hana muda wa kuwaelezea mipango ya kazi.

Hata anapofanyiwa jambo zuri hajui kutoa shukurani anaona alistahili kufanyiwa hivyo yakiwemo mambo mengine  yanayofanana na hayo.

Mbunge wa Jimbo la Babati Mjini Mhe Emmanuel Khambay ni kiongozi bora mwenye maono kwa jinsi anavyoshirikiana na wananchi na viongozi wenzake mbalimbali kuhakikisha wana Babati wanapata maendeleo.

Khambay ni mtu wa watu kiongozi anayejua kushukuru, wakati wote walipo wananchi kwenye shughuli za maendeleo, furaha na huzuni hakosekani.

Mhe. Khambay Januari 4,2026 alishiriki kikao maalum cha Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), Wilaya ya Babati Mjini ambapo alitumia fursa hiyo kuwashukuru wajumbe wa kikao hicho kwa niaba ya wananchi kwa ushindi uliokipata chama hicho  katika uchaguzi mkuu wa 2025.

Aidha, katika kikao hicho alitoa taarifa ya kazi mbalimbali alizozifanya baada ya kula kiapo cha ubunge ambapo aliomba kuendelea kupewa ushirikiano ili aweze kutekeleza miradi ya maendeleo iliyoainishwa kwenye ilani ya uchaguzi ya CCM ya 2025/ 2030. Mbunge wa Jimbo la Babati Mjini Mhe. Emmanuel Khambay,, akiwashukuru wajumbe wa kikao hicho.Viongozi wakiwa meza kuu kwenye kikao hicho.Wajumbe wakiwa kwenye kikao hicho.Kikao kikiendelea

Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wilaya ya Babati Mjini, Elezabeth Malley, akizungumza kwenye kikao hicho.
Mbunge Khambay akisisitiza jambo kwenye kikao hicho. Kutoka kushoto ni Diwani Viti Maalumu Wilaya ya Babati Mjini, Salome Masasi, Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya, Mhe. Yona Wao na kulia Mwakilishi wa CCM.

Taarifa hii imeandaliwa na Dotto Mwaibale 0754362990

Chanzo (Nick- Studio) 

No comments