NIRC YAKABIDHI MRADI WA UMWAGILIAJI WA ZAIDI YA BILIONI 5 KWA MKANDARASI NJOMBE
Na Mwandishi Wetu, Njombe
TUME ya Taifa ya Umwagiliaji (NIRC), imemkabidhi mkandarasi kazi ya ujenzi
mradi wa umwagiliaji katika Kijiji cha Itipingi Mkoani Njombe ambao utagharimu
zaidi ya shingi bilioni 5.2.
Mradi huo awali ulijengwa kwa gharama ya shilingi milioni 400.
Akizungumza baada ya makabidhiano hayo Mkuu wa Mkoa wa Njombe Antony Mtaka ameiagiza halmashauri ya wilaya ya hiyo kuweka mazingira
wezeshi kwa wakulima wa na kutumia mradi huo ipsavyo.
Amesisitiza umuhimu wa kutunza mazingira ya mradi mradi ikiwemo kupima
mashamba na viwanja.
Pia, kuandaa teknolojia za kisasa za kilimo Pamoja na kuandaa masoko ya
uhakika wa mazao yatakayo zalishwa kutoka eneo la mradi.
Akizungumza na wananchi wa Kijiji cha itipingi Mtaka amewaasa wananchi kuutunza mradi huo kwa kuacha kupeleka mifugo
katika eneo la mradi huku akionya vijana
wanaojihusisha na kamari kuacha wizi wa vifaa na uvivu.
Naye Mhandisi wa Tume Mkoa wa Njombe Machage Mwema, amesema baada ya
usanifu wa pili,mkataba wa ujenzi huo
ulisainiwa baina ya serikali na mkandarasi kutoka kampuni ya Sihotech
Engeneering Company ltd na Amj Global Multi contractor co ltd; June 24 mwaka 2024 jijini Dodoma.
Ameeleza shughuli ambazo mkandarasi
huyo atafanya kwa kipindi cha miezi 14 ya ujenzi wa mradi kuwa ni Pamoja na kukarabati miundombinu iliyojengwa kwenye ujenzi wa awali,kundeleza
na kujenga mfereji mkuu, kujenga mifereji ya umwagiliaji,kujenga bara bara za
kuzunguka mashamba,ujenzi wa madaraja ,vivusha maji , kujenga bara bara kutoka
eneo la mradi mpaka kijijini kwaajili ya kusafirisha pembejeo na mazao; na
kujenga ofisi ya mhandisi wa umwagiliaji.
Pia amesema kutokana na ukubwa wa
mradi serikali itanunua gari moja kwajili ya kuhudumia mradi na
kwamba kazi ya ujenzi huo inaanza siku
14 baada ya mkandarasi kukabidhiwa kazi na kuwa mradi huo unalenga kuwahudumia
wakulima 417, idadi ambayo inaongezeka kutoka
wakulima 77 walio tarajiwa katika mradi wa awali.Wanufaika wa mradi
watatoka vijiji vya Itipingi, Kiumba na Malombwe, halmashauri za makambako na
Njombe.
Kwa upande wa wananchi wa Kijiji cha Itipingi wakiongozwa na diwani wa kata hiyo ya Igongolo Isaya Myamba, wameishukuru serikali kwa kutoa fedha za kujenga mradi huo kwa mara ya pili na wameeleza kiu yao ya kunufaika na mradi kwa kuzalisha mazao ya mboga mboga kwa wingi.Makabidhiano ya mradi huo yakifanyikaFuraha ikitamalaki wakati wa makabidhiano ya mradi huo.
No comments