RAIS MWINYI ALIVYOONGOZA KILELE CHA MAADHIMISHO YA MWAKA MPYA WA KIISLAMU
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dkt.Hussein Ali Mwinyi akiongoza kilele cha maadhimisho ya mwaka mpya wa Kiislamu mwaka 1446 Hijriya katika Msikiti wa Jamiu Zinjibar Mazizini, Mkoa wa Mjini Magharibi tarehe 6 Julai 2024.
............................
Na Mwandishi Wetu, Zanzibar
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa
Baraza la Mapinduzi Alhaj Dkt.Hussein Ali Mwinyi amewahimiza wazazi, walezi,
walimu na taasisi zote za elimu kutilia mkazo suala la kuenzi Maadhimisho ya
mwaka mpya wa Kiislamu ili vizazi na jamii iweze kutambua mila na desturi.
Alhaj Dkt.Mwinyi ameyasema hayo wakati wa kilele cha maadhimisho ya mwaka
mpya wa Kiislamu mwaka 1446 Hijriya katika Msikiti wa Jamiu Zinjibar Mazizini,
Mkoa wa Mjini Magharibi tarehe 6 Julai 2024.
Aidha Alhaj Dkt.Mwinyi amesema suala la kutunza na kudumisha amani na
utulivu ni kiini cha mafanikio ya nchi yoyote duniani na amewaomba waumini wa
dini ya kiislamu kuendelea kuitunza amani kama ilivyoamrishwa na Mola Mtukufu
katika kitabu chake kitukufu.
Halikadhalika Alhaj Dkt.Mwinyi amewaomba wafanyakazi wote, wafanyabiashara
wakubwa na wadogo kuongeza bidii katika kazi kwa madhumuni ya kuinua uchumi wa
nchi na ustawi wa watu.
Kwa upande mwingine Rais Dkt.Mwinyi ameipongeza na kuishukuru Ofisi ya
Mufti Mkuu wa Zanzibar kwa kuandaa maadhimisho ya mwaka mpya wa Kiislamu na
kutekeleza majukumu yake.
No comments