WATANZANIA WATAKIWA KUILINDA TUNU YA AMANI.
………………..
Na Hellen Mtereko, Mwanza.
WATANZANIA wametakiwa kulinda amani na utulivu wa nchi kwa kuwa ndio msingi
wa maendeleo.
Wito huo umetolewa na Mratibu wa Mkutano wa Injili utakaofanyika nchini
Tanzania Nabii Utukufu Kwa bwana Peter, wakati akitoa taarifa ya maandalizi ya
Mkutano huo utakaoanza Julai 24, hadi 28 2024 katika uwanja wa michezo wa CCM
kirumba uliopo Wilaya ya Ilemela Mkoani Mwanza.
Amesema kuwa amani tuliyonayo ni tunu kubwa sana inayoweza kutupa furaha
wakati wote na lengo la Mkutano huo ni kuliombea Taifa la Tanzania ili amani
izidi kutawala.
” Taifa hili linamuhitaji Mungu sana na
silaha yoyote inatengenezwa wakati wa amani,hivyo maombi yanayoweza
kutusaidia kwenye Taifa letu ni maombi tunayoweza kuyaomba tukiwa kwenye amani
na utulivu”, amesema
Amesema Maandalizi ya Mkutano utakaongozwa na Pastor Ezekiel Odero wa
Kanisa la New Life Prayer Center kutoka Mombasa Nchini Kenya yanaendelea vizuri
kwaajili ya kuhakikisha watu watakauohudhuria wanapata huduma stahiki.
“Matumaini yetu tunaamini watu wengi watafika katika Mkutano huu na
mpaka sasa tumeishanza kupokea simu
kutoka kwa mataifa mengine juu ya ujio wao kwenye mkutano huu” Amesema Utukufu
Baadhi ya wananchi wameeleza kuwa wanaamini ujio wa Mkutano huo utawapa
uponyaji na kuwafungua kiroho na kupata majibu ya matatizo yao ya muda mrefu.
“Tunaamini ujio wa huyu mchungaji ni faraja kwetu maana tumekuwa tukiangalia kwenye tv na kuona namna watu wanavyoponywa na kufunguliwa kwa maombi na sisi tunaimani hiyo ya kutatuliwa matatizo tuliyonayo hususani ya kiafya”
No comments