WATANZANIA WAASWA KUTOA MAONI YAO DIRA 2050
Makamu wa Pili wa Rais wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Mhe. Hemed Suleiman Abdulla, akizungumza na Wajumbe wa Tume ya Mipango na Timu Kuu ya Wataalamu ya Dira ya Taifa 2050 ofisi kwake.
................................
Adelina Johnbosco, Zanzibar
Makamu wa Pili wa Rais wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Mhe. Hemed
Suleiman Abdulla, amewataka Watanzania wote kushiriki kikamilifu katika zoezi
la kutoa maoni yatakayowezesha kuandaliwa kwa Dira ya Taifa 2050.
Ametoa rai hiyo leo Agosti 28, 2024, ofisini kwake mjini Magharibi wakati
akiongea na wajumbe wa Tume ya Mipango na Timu Kuu ya Wataalamu ya Dira ya Taifa 2050 iliyoongozwa na mjumbe
wa Tume ya Mipango na Mwenyekiti wa Timu hiyo, Dkt. Asha Rose Migiro.
“Watanzania wote waendelee kutoa maoni yao ili tuweze kupata Dira
tunayoitaka, asitokee mtu tukishapata Dira akasema sikupata fursa ya kutoa
maoni, makundi yote waone umuhimu wa kushiriki kutoa maoni, hili ni jambo
muhimu na lenye manufaa katika kuisaidia nchi yetu,” alisisitiza Mhe. Abdulla
Vilevile, amehimiza ulazima wa kila Mtanzania kuhakikisha anadumisha amani
na utulivu ili mipango ya maendeleo ya Dira 2050 iweze kutekelezwa kikamilifu.
Katika hatua nyingine, Mhe. Abdulla, amewakaribisha Wananchi wote
katika Chuo Kikuu cha Taifa cha
Zanzibar (SUZA), siku ya Jumamosi Agosti 31, 2024, ili kushiriki katika
kongamano la kutoa maoni kwa ajili ya Dira ya Taifa 2050 ambapo mgeni rasmi
anatarajiwa kuwa Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mhe. Hemed Suleiman
Abdulla.
No comments