Breaking News

USIKU WA GUMI LA DHAHABU' WATIKISA PANGANI.

Na Mashaka Kibaya. Pangani 

MKUU wa Wilaya ya Pangani Gift Msuya ameahidi kufanya kila jitihada kuhakikisha mchezo wa ngumi unakwenda kuipaisha wilaya hiyo na kuitangaza kitaifa na hata katika medani za Kimataifa.

MKUU huyo ametoa Kauli hiyo jana (02/11/2024) alipokuwa mgeni rasmi kwenye tamasha la mchezo wa ngumi lililopewa jina la usiku wa 'Gumi la dhahabu', pambano ambalo limefanyika katika ukumbi wa Pangadeco Beach Hotel.

Wilaya ya Pangani kupitia Pangani Boxing Promotion  imeendesha mpambano huo wa ngumi za ridhaa kwa lengo la kuhamasisha Wananchi kujitokeza kwa wingi kupiga kura kwenye uchaguzi wa Serikali za Mitaa ifikapo Novemba 27 mwaka huu.

Katika hotuba yake ya ufunguzi wa mchezo huo,Mkuu huyo wa wilaya Gift Msuya,alisema kwamba atashirikiana na ofisi ya Mbunge wa Jimbo la Pangani Jumaaa Hamidu Aweso kuibua na kulea vipaji na hivyo vijana wanaocheza mchezo huo kufika kwenye medani za Kimataifa.

"Tunataka wageni waje kujifunza Pangani na tupate vipaji tutakavyovipeleka Duniani na Pangani iweze kujulikana zaidi.Washindi tutawapromoti waende kushindana mashindano ya Kitaifa na Kimataifa ili kwenda kuonesha vipaji vyao na kuitangaza Pangani yetu" alisema Mkuu wa Wilaya.

Tamasha hilo la ngumi lilikuwa na mapambano Tisa (9) yaliyowashirikisha Vijana mabondia wa Wilaya ya Pangani na wale wa kutoka Halmashauri ya Jiji la Tanga ambao waliweza kuibuka kidedea licha ya wenyeji ambao walioonekana kuwa wachanga kwenye masumbwi kuweza kutoa upinzania mkali.

Aidha Mkuu wa Wilaya Gift Msuya amemtaja Rais Dkt Samia Suluhu Hassan kwamba Kiongozi mwenye upendo kwenye sekta ya michezo ambaye amekuwa akifanya hamasa kubwa ya kuwazawadia wanamichezo.

"Rais Dkt Samia hoyeee... hapa unajua kwanini nini nimemtaja.Ni kwa sababu amekuwa akifanya makubwa hasa kutoa hamasa kwenye michezo anatoa fedha nyingi.Hata leo nilikuwa napitia 'comment' social media comment ya kwanza ya kwake juu ya Azam kuifunga Tanga hapa anadhihirisha timu zote ni zake"alisema DC Gift.

Katika mpambano huo DC Gift alichangia Shilingi 500,000 kwa Pangani Boxing Talent waandaji wa tamasha hilo la ndondi ili kuwawezesha kufanikisha mchezo huo ambao wahusika walimueleza kukabiliwa na ukata wa fedha.

Hata hivyo Mkuu wa Wilaya Gift Msuya alitumia fursa hiyo kuwahimiza Wananchi wote kujitokeza kwa wingi kupiga Kura hapo Novemba 27 mwaka huu alisema,hiyo ni hatua muhimu katika kuwapata viongozi kwa ajili ya kusimamia maendeleo yao.

No comments