WATURUKI ZANZIBAR WADAIWA KUTUMIA YATIMA KUJIPATIA MAMILIONI YA FEDHA
Na Mwandishi
Wetu, Zanzibar
RAIA wa
Kituruki wanaoendesha Taasisi ya The Institute of
Holistic Education of Zanzibar
inayomiliki Sekondari ya Bweni ya Wavulana ya Olgun iliyopo Mkoa wa Magharibi “B”, Zanzibar wanadaiwa kuingia katika kashifa
ya kujipatia mamilioni ya fedha kupitia yatima.
Uchunguzi
uliofanywa na mwandishi wa habari hizi umebaini kuwa waturuki hao wamekuwa
wakiwapiga picha watoto hao wakiwa kwenye makazi duni na kuwatumia wafadhili
hao ambao huwatumia fedha.
Mmoja wa
aliyekuwa mfanyakazi wa taasisi hiyo aliyejitambulisha kwa jina la Salim Hamad
Mbaruku akizungumza na waandishi wa habari alisema mambo yanayofanyika ndani ya
taasisi hiyo ambayo pia inafundisha elimu ya dini kwa watoto wa madrasa ni
kinyume kabisa na misingi ya dini hiyo.
Mbaruku alisema
tangu ianzishwe taasisi hiyo imeweza kujenga shule hiyo kwa gharama kubwa
kupitia ufadhili wa watu wa Uturuki ambao wanaamini wanasaidia yatima wa Zanzibar
ambao wanatozwa ada kubwa wakati ilipaswa wasome bure.
Mbaruku
alidai viongozi wa taasisi hiyo wamekuwa
wakisaidiwa na baadhi ya wanzanzibar ambao sio waaminifu kufanya vitendo hivyo
ambapo wamefikia hatua ya kujenga vibanda vya nyasi katika eneo la taasisi
hiyo na kuwapiga picha watoto hao mbele ya vibanda hivyo na kuzituma kwa
wafadhili hao na kuwafahamisha watoto
hao yatima huishi kwenye vibanda hivyo.
Wafadhili
hao baada ya kuziona picha hizo huwaonea huruma watoto ambao sio yatima na
kutuma mamilioni ya fedha ili wajengewe makazi bora ya kuishi fedha zinazoishia
mifukoni mwa wajanja hao.
Mbali ya
kujenga vibanda hivyo, inadaiwa wakati
wa Mfungo wa Mwezi Mtukufu wa Ramadhani viongozi wa taasisi hiyo huwatuma
baadhi ya wafanyakazi wao kwenda kuwachukua watoto majumbani mwao kwa ajili ya kuwapa
futari.
Inadaiwa kuwa katika kila sahani ya futari wanayopewa huwekwa nanasi zima na kupigwa picha, baada ya
zoezi hilo mananasi hayo huondolewa bila kuliwa.
Inadaiwa picha
hizo zinatumwa Uturuki kwa wafadhili na kueleza taasisi hiyo imekuwa ikitoa mlo
kamili kwa watoto hao.
Mbaruku anayedai
kufanya kazi ya mwalimu wa madrasa kwenye taasisi hiyo kwa miaka mitano alisema
alikuwa akilipwa Sh. 150,000 na kusainishwa kwa jina la mtu mwingine anayeitwa Salim
Othman na hata alipohoji wahusika walikuwa hawampi majibu ya kueleweka zaidi ya
kumueleza kuwa alikuwa akipewa fedha hizo kama sadaka tu na si vinginevyo.
“ Hali sio
nzuri kwenye taasisi hiyo tunajiuliza hivi watanzania wanaweza kufanya mambo ya
namna hii huko Uturuki na mamlaka
zinazohusika zipo kweli kwa sababu mambo haya yanafanyika hapa Zanzibar bila ya
kificho tunaomba watu wa Ustawi wa Jamii, Wizara ya Elimu wafuatilie haya mambo,” alisema Mbaruku kwa
masikitiko.
Mbaruku alisema
hata watu wa Idara ya Uhamiaji wanapaswa kufika kwenye taasisi hiyo kujua
uhalali wa vibali vya kuishi na kazi ambazo wameziainisha waturuki hao.
Inadaiwa
wafanyakazi wanapodai kupewa mikataba ya kazi huambiwa waende popote pale hata
huko juu hawatapata msaada kwa sababu taasisi hiyo ina mtandandao mkubwa wa
watu wa kuwasaidia serikalini na baadhi ya viongozi wakubwa wa dini.
Mbruku
alisema licha ya kuwataka viongozi hao wampe haki yake baada ya kumuachisha
kazi wamegoma na kusisitiza kuwa hakua mfanyakazi wao kwa kuwa hana mkataba.
Aliongeza
kusema , katika hali ya kushangaza Novemba 5, 2024 alipofika kudai haki yake
mmoja wa kiongozi wa taasisi hiyo alimkabidhi barua iliyoandikwa Septemba 28, 2024
ambayo mwandishi wa habari hii anayo nakala yake iliyoandikwa hivi:
“ Mheshimiwa
Salum Mbarouk Othman, Taasisi yetu imekuwa ikitoa msaada wa kifedha kwa muda
mrefu ili kusaidia shughuli zako za dini ya Kiislamu. Hata hivyo, kufuatia
tathimini iliyofanywa, baraza la uongozi limeamua kusitisha msaada wa kifedha
kwako kwa sababu ya kukosa kuzingatia kwa umakini mahitaji ya Kiislamu”
ilisomeka barua hiyo iliyosainiwa na Mwenyekiti wa taasisi hiyo
aliyejitambulisha kwa jina moja la Ibrahim.
Aidha,
Mbaruku alisema sababu ya kuachishwa kazi imetokana na uongozi wa taasisi hiyo
kumtaka aende akasimamie madrasa na msikiti uliopo eneo la Maungani ambapo alitaka waandikiane mkataba kwa kazi
hiyo mpya sambamba na nyumba aliyoahidiwa angekaa bure na familia yake.
“Nilimuambia
boss Ibrahim kuwa kama ananihitaji kunihamishia Maungani baada ya kuridhishwa na
kazi nzuri nilioifanya kwenye madrasa ya awali nahitaji anilipe shilingi laki
nne ili ziniwezeshe kukidhi mahitaji ya familia yangu hivyo anipe mkataba ambao
utaelezea nyumba nitakayo kaa nitaishi bure ili nisije nikasumbuliwa baadae,”
alisema Mbaruku.
Mbaruku
alisema baada ya kumuambia hivyo boss wake huyo alikasirika na kuchukua uamuzi
wa kumuondoa kazini na hiyo ndio sababu ya kutokea kwa chokochoko zote hizo na
sio kukiuka taratibu za dini ya kiislamu alizozitoa kwenye barua
aliyokabidhiwa.
Akizungumza
na waandishi wa habari kwa njia ya simu Kaimu Mkurugenzi wa Taasisi hiyo Abii
Rashid Rashid alikiri kumfahamu Mbaruku ambapo alikana hakuwa mfanyakazi wa
taasisi hiyo.
“Mbaruku sio
mfanyakazi wetu kwa sababu hana mkataba kama anao awaonesheni hapa alikuwa
anafanya kazi za kusaidia kufundisha madrasa sisi tulikuwa tunampa hela kama
sadaka na kama anataka kuchafua taasisi yetu tutamshitaki yeye na vyombo vya
habari kwa sababu taasisi yetu ni kubwa na ipo dunia nzima na tunawanasheria
wetu,” alisema Rashid.
Watoto wakipata chakula na juu ni vibanda vinavyodaiwa kujengwa na taasisi hiyo ambavyo watoto hao hao upigwa picha na kuzituma kwa wafadhili wa kituruki wakielezwa ndivyo vinavyotumiwa kulala watoto hao wakati sio kweli.
Muonekano wa majengo ya shule yaliyojengwa na taasisi hiyo.
No comments