MBETO : JUSSA FUTA NDOTO ACT WAZALENDO KUINGIA IKULU
........................................
Na Mwandishi Maalum , Zanzibar
CHAMA Cha Mpinduzi (CCM) kimesema kwa vyovyote ACT
Wazalendo hakina wezo wa
kuishinda CCM na kumuondoa Rais aliye
madarakani Zanzibar Dk Hussein Ali
Mwinyi.
Pia kimemkanya Makamu Mwenyekiti wa
ACT Wazalendo, Ismail Jussa Ladhu,
kutoidanganya dunia, kuwapa matuimaini
hewa wafuasi wao kwa kufikiria mambo yasiowezekana.
Onyo hilo limetolewa na Katibu wa Kamati Maalum ya NEC Zanzibar ,Idara ya Itikadi, Uenezi na Mafunzo , Khamis Mbeto Khamis , alipokijibu madai yaliotolewa na Jussa katika mkutano wa hadhara uliofanyika Kibandamaiti Kisiwani Unguja.
Mbeto alisema CCM hakijawahi kuwa na nakisi ya kura zake za ushindi mwaka 2025 ,pia
si wana CCM Zanzibar au Tanzania , wanaoupinga utawala
aidha wa
Rais Dk Samia Suluhu Hassan au Rais Dk. Mwinyi .
Alimtaja Jussa ndiye asiyekubalika
ndani ya ACT kutokana na aina ya uongozi wake uliokigawa chama hicho kati ya viongozi waasisi na wapya .
"Jusa amejitumia ujumbe unaohusu
aina ya uongozi na siasa
zisizokubalika ndani ya ACT. Aache
kujenga himaya mpya ma kuwagawa watu.
Asitake sauti yake iwe uamuzi
kuliko vikao na katiba ya ACT "alisema Mbeto.
Alisema CCM kina taarifa za
kutosha za kiongozi
huyo asivyokubalika , alivyojipanga
kuunda ACT a ndani ya ACT huku
akiishi kwa kupigiwa debe na mjane wa Hayati Maalim Seif
Mama Awena Sinani .
"Jussa hatakiwi ndani ya ACT .Anaishi kwa ushawishi na
heshima ya Mama Awena.
Wenzake hawamtaki kwa jeuri , kibri na
kujifanya kwake kujua kila kitu .Jussa hawezi kuwachagulia Rais wazanzibari
wasiyemtaka" alisema.
Aidha Katibu huyo Mwenezi
CCM Zanzibar, alisema Jussa
asidhani kama atamudu kuvivaa viatu
vilivyoachwa na Maalim seif sharif Hamad vikamtosha kwa ujuvi alionao , kutoambilika huku akikwepa kuoa.
'Mfikishieni salamu jussa aache
kujifanya anajua wakati yeye mwenyewe
hajijui . Wenzake wamemsusa wakitaka
abaki na kundi la wahamiaji .
Kumtenga Juma Duni Haji na waasisi
wengine kumewakera wengi Act "
alieleza.
No comments