MBETO: WANAMICHEZO ZANZIBAR WAKATI NI HUU
........................................
Na Mwandishi Maalum , Zanzibar
Chama Cha Mapinduzi (CCM )
kimewataka wanamichezo Zanzibar , kuchangamkia fursa zilizopo katika utawala wa SMZ awamu ya nane kuweka bidii na kuonyesha vipaji vyao ili kuwa kucheza ngazi za kimataifa.
Ushauri huo umetolewa na Katibu wa Kamati
Maalum ya NEC Zaanzibar ,Idara ya Itikadi
,Uenezi na Mafunzo, Khamis Mbeto
Khamis wakati kabla ya kuanza mechi ya fainali ya kombe la
Abdulghafar jimbo la Mtoni Mkoa Mjini Magharibi.
Jimbo la Mtoni linaoongozwa na Mbunge
wake Abdulghafar Idrisa
Mbeto alisema wanamichezo wote katika uongozi wa Rais wa Zanzibar Dk Hussein
Ali Mwinyi, wamepata bahati ya
kujengwa viwanja vya kisasa vya soka
huku Rais akiwa ndiye mdau Mkuu wa
Michezo.
Alisema kila akitazama kwa wakati
huu ,anatamani ingerudi enzi
ya kushamiri kwa viwango
soka zanzibar kwa timu kama
Mwembelendu, Miembeni Vikokotoni,
Ujamaa, Navy na Kikwajuni.
Timu nyingine zilizokuja kuwika baadae
Malindi, Black Fighters, Jamhuri, Small Simba, Shangani na Mlandege huku akisema Zanzibar ingepata soko la kuuza wachezaji
wake wengi duniani.
Mbeto alisema hata hivyo zanzibar
bado ina nafasi kubwa kwa wachezaji wake kujutuma na kutumia nafasi
zilizopo kujijenga kiuchumi kupitia soka, kuogelea, riadha ,masumbwi na
michezo mingine kadhaa.
"Serikali imefanya kila linalowezekana na Zanzibar inatambuliwa na caf .Itatacheza michuano ya
cecafa kama Zanzibar . Ukitambuliwa Cecafa
umetambuliwa Fifa. Wales,
Scotland, Northern Island na
England zinacheza kombe la dunia zikiwa
nchi za Muungano UK, " alisema Mbeto.
Aidha Katibu huyo Mwenezi, alisema CCM kitaendelea kusimamia sera
zake katika kuinua michezo
ili kuwafanya wanamichezo waishi
maisha bora kupitia jasho na vipaji vyao.
Hata hivyo alisema chama kimeielwlza SMZ kupitoa waziri wake dhamana ya
michezo , kupeleka wanamuziki wa taarab asilia kwenye nchi za Misri na UAE ili kuongeza mbinu na ujuzi wa
muziki huo .
"Huwezi kuitenganisha Zanzibar na muziki wa taarab .Maisha ya watu wake na
mioyo yao huburudika kwa muziki wa taarab ulioipa sifa Zanzibar kona zote duniani "alisema
Mbeto.
No comments