Breaking News

PRADO YAPATA AJALI YAWAKA MOTO YAUA WATU SITA WAKIWEMO WALIMU WANNE RUVUMA

Wananchi wakiangalia ajali ya gari aina ya aina ya Prado lenye namba za usajili T 647 CVR, mali ya Vicent Alel Milinga mkazi wa Kijiji cha Lumalu lililopata ajali , Kata ya Upolo, Wilaya ya Nyasa mkoani Ruvuma na kusababisha vifo vya watu sita.

................................ 

Na Regina Ndumbaro- Ruvuma 

Watu sita wamefariki dunia katika ajali ya gari iliyotokea katika Wilaya ya Nyasa, mkoani Ruvuma.

Ajali hiyo imetokea Desemba 28, 2024, wakati ikisafiri kutoka Kijiji cha Lumalu kilichopo katika Kata ya Upolo kuelekea makao makuu ya wilaya.

Akizungumza kwa njia ya simu, Mkuu wa Wilaya ya Nyasa, Peres Magiri, amethibitisha kutokea kwa ajali hiyo, ambayo imesababisha vifo vya walimu wanne  wa Shule ya Msingi Lumalu.

Watu wengine waliofariki katika ajali hiyo ni dereva wa gari hilo  Vicent Alel Milinga na mtu mwingine aliyetajwa kwa jina la  Boniface Mapunda.

Gari lililohusika katika ajali hiyo ni aina ya Prado lenye namba za usajili T 647 CVR, mali ya Vincent Alel Milinga mkazi wa Kijiji cha Lumalu, Kata ya Upolo, Wilaya ya Nyasa.

Walimu waliopoteza maisha katika ajali hiyo ni Damas Damasi Nambombe ,Domenica Abeat Ndau ,Judith Joseph Nyoni na John Silvester Mtuhi.

No comments