Breaking News

YAZID MABALA MHANDISI ANAYEWIWA KUIONA MWIBARA IKIWA KINARA KWA MAENDELEO- BUNDA MKOANI MARA

 Mhandisi  Yazid Mabala Mdau wa Maendeleo Mkoa wa Mara

.........................


UZALENDO ni hali ya mtu kuipenda, kuithamini na kujitoa kwa ajili ya nchi na  Mzalendo wa kweli wakati wote anaweka maslahi ya nchi na ya jamii mbele. 

Uzalendo unabeba dhana pana ikianzia asili, utamaduni, lugha, siasa, historia zote zikifungwa kwenye dhana kuu ya utaifa.

Katika Taifa la Tanzania kumekuwepo na wazalendo wengi, baadhi wamekwisha tangulia mbele za haki akiwemo aliyekuwa Rais wa Kwanza wa Tanzania Hayati Julius Kambarage Nyerere, Hayati Abeid Amani Karume, Hayati Rashid Mfaume Kawawa, Hayati Edward Moringe Sokoine, Hayati Edward Ngoyai Lowassa, Hayati Bibi Titi Mohamed na wengine wengi.

Leo napenda kumuongelea Mhandisi  Yazid Mabala ambaye ni Mdau wa Maendeleo aliyejikita kuleta chachu ya mapinduzi ya maendeleo ndani ya Mwibara, Bunda Mkoa wa Mara ni Kada wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) anayewekeza katika kuwatumikia Wananchi wote na Watanzania kwa ujumla bila ubaguzi na anaeziishi 4R za Mhe Dkt Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania (JMT) na Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Taifa  kwa Vitendo.

Katika upande wa utunzaji wa Mazingira nchini, Mhandisi Yazid Mabala ametoa mchango mkubwa wa Utunzaji wa Mazingira kwa kutoa miche ya miti 5,000 ikiwa ni miche ya miti mchanganyiko ndani ya Mwibara-Bunda, Mara ili kuhakikisha Tanzania inaendana na kukabiliana na mabadiliko ya Tabianchi kutokana na Sera ya Umoja wa Mataifa ya utunzaji Mazingira.

Aidha, Mhandisi Mabala katika kuinua sekta ya Michezo amekuwa mstari wa mbele kuchangia kutokana na Umuhimu wa Michezo kwenye jamii kwani Michezo inaleta Umoja, Michezo ni ajira kwa vijana, Michezo ni sehemu ya kujenga afya ya mwili na akili.

Mwaka 2021, 2022, 2023 na Mwaka 2024, Mhandisi Mabala amewezesha Ligi ya mchezo wa mpira wa miguu ndani ya Mwibara ambapo ametoa vifaa vya michezo ikiwemo Mipira, Jezi, Maji na Mbuzi kwa ajili ya mshindi wa mashindano ya Michezo yaliyofanywa chini ya ufadhili wake.

Mwaka 2021 akiwa kama mdau mpenda maendeleo alipata ombi kutoka Chama Wilaya la kuchangia katika uandikishaji wa Wanachama wapya ambapo alifanikiwa kuchangia Simu Janja mbili ili kusaidia Ujenzi wa Chama hicho.

Mwaka 2021  aliwezesha kufanyika kwa kongamano kubwa la kuwajenga Vijana Kifikra katika kujisimamia Kiuchumi na kuziibua Fursa zilizojificha za Uzalishaji ili Vijana hao waendelee kujisimamia wao wenyewe siku zote ndani ya Jimbo la Mwibara na Mgeni Rasmi katika kongamano hilo alikuwa Joshua Nasari aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Bunda wa Kipindi hicho na Mbunge wa Jimbo la Mwibara alipewa Mwaliko pia.

Mwaka 2021 alisaidia katika ujenzi wa darasa katika Shule ya Msingi Muungano kwa  kuchangia trips za Mchanga na mawe katika ujenzi huo.

Hayo yaliyotajwa hapo juu ni baadhi ya kazi chache kati ya nyingi ambazo amezifanya mhandisi huyo kwa ajili ya kusaidia jamii ikiwa ni kuunga mkono jitihada za Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan za kuwaletea wananchi maendeleo.

Mhandisi Mabala wakati akitoa salamu za Sikukuu ya Krismasi na Mwaka Mpya 2025 ameahidi kuendelea kuisaidia jamii  inayomzunguka ili iendelee kujisimamia katika uzalishaji kwa kuwapa mbinu mbalimbali ili kuweza kukuza pato la mtu mmoja mmoja ili waweze kupiga hatua za maendeleo kwani hiyo ndiyo furaha yake kuwatumikia wananchi na Watanzania kwa ujumla bila kujali dini, Kkabila , vyama vyao na  jinsia zao.

Binafsi napenda kuchukua nafasi hii kukutakia mafanikio kwa mipango yako mizuri yenye lengo ya kuisaidia jamii kwani huo ndio uzalendo wa kweli.

Mhandisi Mabala Mungu akupe afya njema ili matamanio yako ya kuwaletea wananchi wa Mwibara maendeleo na yakatimie bila ya kusahau kumuomba Mungu kwani kila penye mafanikio hapakosi changamoto. Kazi Iendelee.

(Makala hii imeandikwa kwa msaada wa ofisi ya Mhandisi Yazid Mabala). kwa mawasiliano ya mwandishi piga namba (0754-362990)

No comments