Breaking News

WAZIRI WA ULINZI NA JESHI LA KUJENGA TAIFA DKT. STARGOMENA TAX AONGOZA MAZISHI YA MEJA JENERALI BUSUNGU

Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa Mhe. Dkt Stargomena Lawrence Tax akitoa heshima za mwisho kwenye jeneza lenye mwili wa marehemu Meja Jenerali Martine Busungu (Mstaafu) wakati wa shughuli ya kuaga mwili huo kabla ya mazishi yake yaliyofanyika Kijiji cha Luchelele Jijini Mwanza Disemba 28, 2024.

............................................

Na Mwandishi Wetu, Mwanza.

WAZIRI wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa Mhe. Dkt Stargomena Lawrence Tax ameongoza Maafisa, Askari, vijana wa JKT, watumishi wa umma na waombolezaji katika mazishi ya  marehemu Meja Jenerali Martine Busungu (Mstaafu) yaliyofanyika Kijiji cha Luchelele Jijini Mwanza tarehe 28 Disemba 2024.

Akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Tanzania Jenerali Jacob John Mkunda katika mazishi hayo, Mkuu wa Jeshi la Kujenga Taifa na Afisa Mtendaji Mkuu wa SUMAJKT Meja Jenerali Rajab Nduku  Mabere amesema, Meja Jenerali Busungu (Mstaafu) akiwa mtumishi ndani ya Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania amelitumikia jeshi kwa kipindi cha miaka thelathini na nne (34), ambapo alikuwa mwaminifu, mtiifu Hodari katika kutekeleza majukumu yake.

Meja Jenerali Busungu Mstaafu) alifariki dunia tarehe 24 Disemba 2024 katika hospitali ya taifa ya Muhimbili Jijini Dar es Salaam

Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa Mhe. Dkt Stargomena Lawrence Tax akiweka shada la maua kwenye kaburi la marehemu Meja Jenerali Mstaafu Busungu.
Heshima za mwisho zikitolewa kwa marehemu.
Watoto wakiweka shada la maua kwenye kaburi la baba yao.
Maafisa wa JWTZ wakiendelea na shughuli za kuaga mwili wa marehemu kabla ya mazishi.
Heshima zikiendelea kutolewa.
Mjane wa marehemu akitoa heshima za mwisho kwa mume wake.
Jeneza lenye mwili wa marehemu likishushwa kaburini.
 

No comments