SHIRIKA LA ENGENDERHEALTH LAIPA KONGOLE SERIKALI
Mratibu wa Shirika hilo Mkoani Tanga Loveness Malisa akizungumza
........................................
Na Mashaka Kibaya
SHIRIKA la EngenderHealth Tanzania limeishukuru Serikali ya Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania kwa kurahisisha upatikanaji wa huduma za afya kwa jamii
ikiwemo ya watu wenye Ulemavu kutokana na hatua yake ya kujenga vituo vingi vya
afya hapa nchini .
Mratibu wa Shirika hilo Mkoani Tanga Loveness Malisa ametoa Shukrani hizo
Jana katika risala yake aliyoitoa kwenye maadhimisho ya siku ya watu wenye
Ulemavu yaliyofanyika kwenye Ukumbi wa YPCP katika Jiji la Tanga.
Licha ya hayo Malisa alisema kwamba wanakutana na changamoto ya uwepo wa
idadi ndogo ya watumishi waliopata mafunzo kuhusu huduma jumuishi na shirikishi
kuhusu Kada ya watu wenye Ulemavu hivyo kuwasababisha kushindwa kufikia
malengo.
Changamoto nyingine ni juu ya uwepo wa mifumo ya ukusanyaji wa taarifa za
afya ambazo zimeshindwa kuwatambua watu wenye ulemavu hali inayokwamisha
kuwafahamu watu wenye ulemavu wanaopata huduma .
Ameishauri Serikali kuweka mafunzo ya huduma shirikishi kwenye mitaala ya
mafunzo kwa wanafunzi wa Kada ya afya sanjari na suala la uboreshwaji wa
miumdombinu kwenye vituo vya afya kuifanya kuwa rafiki kwa walemavu.
Mmoja wa washiriki wa Mkutano huo Salehe Mwaluku ameiomba Serikali
kuangalia uwezekano wa kuendelea kutoa elimu ya ujasiriamali kwa jamii ya watu
wenye Ulemavu hatua ambayo itawawezesha kunufaika na fursa ambazo zinapatikana
nchini kwao.
Amewasilisha ombi hilo wakati akichangia mada kwenye Kongamano hilo lililoshirikisha wajumbe
kutoka vyama vya watu wenye Ulemavu akisema, kuna haja kwa Serikali kuendelea
kutoa elimu ya ujasiriamali
itakayowasaidia kumudu suala la utejeshaji Mikopo ya asilimia kumi.
Maadhimisho ya siku ya watu wenye Ulemavu Duniani hufanyika kila Disemba 3
kila mwaka lengo likiwa kukuza uelewa juu ya haki na ustawi wao na kuhamasisha
jamii kuona umuhimu wa kuwashirikisha walemavu kwenye nyanja zote za maendeleo
kama vile afya.
Malengo mengine ni pamoja na kutathimini maendeleo katika utekelezaji sera
na mikakati ya kuhakikisha usawa na ujumuishi kwa walemavu, pia ni jukwaa
maalum lankuwaonesha watu wenye Ulemavu kuonesha vipaji vyao na kueleza
changamoto wanazokutana nazi katika maisha yao ya kila siku.
No comments