MBETO : UKWELI UKUDHIHIRIKA UONGO HUJITENGA
Katibu wa Kamati Maalum ya NEC Zanzibar Idara ya Itikadi, Uenezi na Mafunzo, Khamis Mbeto Khamis, akizungumza na Waandishi wa habari katika Òfisi Ndogo ya CCM huko Chachani Kisiwani Pemba.
............................................
Na Mwandishi Wetu, Pemba
CHAMA Cha Mapinduzi (CCM)
kimesema zama za ushindani wa siasa usiotoa matokeo chanya, tija wala manufaa kwa jamii zimepitwa na wakati ,badala yake
wananchi wanataka kuona mambo kwa macho na vitendo .
Maneno hayo yamebainishwa na
Katibu wa Kamati Maalum
ya NEC Zanzibar Idara ya Itikadi, Uenezi na Mafunzo ,Khamis Mbeto Khamis, alipozungumza na Waandishi wa habari
katika Òfisi Ndogo ya CCM
huko Chachani Kisiwani Pemba.
Mbeto yupo Kisiwani
Pemba kuhudhuria Sherehe za
Maadhimisho ya Miaka 61 ya
Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar .
Alisema kadri siku zinavyozidi kwenda
mbele ,toka kizazi kimoja hadi kingine , wananchi wa Zanzibar
,wamekuwa wakibadilika polepole
huku wakiachana na siasa za kukaririshwa mambo yasio fikirika.
"Zile zama za watu kukaririshwa
au kulishwa maneno yenye siasa za sumu
, chuki na hasama ,zinaelekea
kufikia tamati . Kila mtu
zanzibar sasa ameamka ,anataka kushuhudia kwa vitendo na kuona kwa macho
yake " alisema Mbeto.
Katibu huyo mwenzi ,alisema utawala
wa Rais Dk Hussein Ali Mwinyi
tokea ashike madaraka, amekuwa kiongozi wa vitendo, asiyeamini katika hadithi za kufikirika zisizoipatia
jamii manufaa na matunda ya
maendeleo .
'Hatutaki siasa domo mtindi samli kwa mwenye ng'ombe. Wananchi ni werevu wangependa kuona
vitendo na kwa macho yao. Simulizi za nikipata nitafanya hazina nafasi
. Watu wanataka kuona aliye madarakani
anafanya nini na kuonekana" alieleza Mbeto
Aidha Katibu huyo
mwenezi amewashauri Waandishi wa
vyombo mbalimbali vya habari
waliofika pemba kabla au baada ya sherehe za Mapinduzi
,waitembelee pemba na kushuhudia ustawi mpya wa maendeleo
.
'Mwaka 2025 ni Mwaka wa kufunguliwa
milango ya kiuchumi na ongezeko la kasi ya maendeleo pemba. Utajengwa uwanja wa kisasa wa Ndege Chakechake . Bandari za
Mkoani, Wesha na Wete " alisisitiza.
Mbeto alisema kuna ujio wa
Wawekezaji wa ndani na nje ambao watajenga Viwanda Vidogo ;Vya kati na
Vikubwa Unguja na Pemba .SMZ imepania kuimarisha sekta ya Uvuvi kwa kununua meli zitakazofika masafa ya mbali baharini.
Pia aliwatolea wito wanamichezo kisiwani Pe mba ,wakiwemo
wanasoka, wanariadha, wachezaji wa mpira
wa pete, masumbwi , kuogelea ,wasanii wa
muziki wa kizazi kipya na taarabu ,kuonyeaha
vipaji vyao na kufikia ngazi za
kimataifa.
'Siku zote ukweli ukidhihiri uongo utajitenga. Vitendo hunena kuliko maneno
. Waacheni wapinzani wetu wabeze
maendeleo yaliopo huku wananchi
wakijionea yote yanayofanyika"
Alieleza Mwenezi huyo.
No comments