Breaking News

MASAUNI : BIASHARA YA KABONI BI UKOMBOZI KWA TAIFA

 Atembelea kituo cha Taifa cha ufuatiliaji Morogoro. 

 DC Shaka Morogoro imejipanga na iko tayari kutumia fursa.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira, Mhandisi Hamad Yussuf Masauni akizungumza alpotembelea Kituo cha Taifa  cha Ufuatiliaji  wa Kaboni (NCMC) nchini kilichopo mkoani Morogoro. Kushoto ni Mkuu wa Wilaya ya Kilosa  Shaka Hamdu Shaka.

................................................
Na Mwandishi Wetu, Morogoro 

WAZIRI wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhandisi Hamad Yussuf Masauni  amesema  kituo cha Taifa  cha ufuatiliaji  wa Kaboni (NCMC) nchini kilichopo Mkoani Morogoro kitakuwa  ni miongoni mwa taasisi muhimu nchini katika kusaidia Taifa kutokana na  miradi mbali mbali ambayo  mataifa ya nje yanakuja kuwekeza kupitia biashara ya Kaboni, ili biashara hiyo iweze kusaidia katika kukuza kipato cha  wananchi lakini pia kuchangia uchumi wa nchi kwa ujumla.

Ameyasema hayo leo alipofanya ziara ya kutembelea kituo hicho kilichopo mkoani Morogoro.

Mapema Mkuu wa Wilaya ya Kilosa  Shaka Hamdu Shaka ambae alimuwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Morogoro katika ziara hiyo  amesema mkoa huo umejipanga kutumia vyema fursa hiyo ili kutekeleza na kutafsiri kwa vitendo maelekezo na  maono ya Rais Samia ya kuhakikisha  biashara ya Kaboni inakuwa vyenzo vyengine ya kuinua kipato cha wananchi na kuchangia katika maendeleo nchini.

"Ni fursa muhimu sana kwetu uwepo wa kituo hiki mkoani kwetu ni hatua muhimu sana, kwani vianzio vyote vinavyopelekea biashara hii kufanyika tunavyo kupitia misitu, mifugo na  mito tutahakikisha fursa hii inatumika vyema na tija iweze kuonekana kwa wananchi na Taifa kwa ujumla kupitia rasilimali tulizonazo,"  alisema Shaka.

Mkuu wa Wilaya ya Kilosa  Shaka Hamdu Shaka.
Mazungumzo na Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira, Mhandisi Hamad Yussuf Masauni yakifanyika wakati wa ziara yake mkoani humo
Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira, Mhandisi Hamad Yussuf Masauni akiagana na wenyeji wake tayari kwa kuendelea na ziara yake.
 

No comments