PROFESA KABUDI AVIPONGEZA VITUO VYA REDIO
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Profesa Palamagamba Kabudi (katikati) akiwa na viongozi wengine wakati akifungua mkutano mkuu wa watoa huduma za Utangazaji 2025 uliofanyika Februari 13, 2025, Kutoka kushoto ni Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Maudhui TCRA, Saida Muki, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Rosemary Senyamule, Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), Dkt. Jabir Bakari na Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo ambaye pia ni Msemaji wa Serikali, Geryson Msigwa.
...................................
Na Dotto Mwaibale, Dodoma
WAZIRI wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Profesa
Palamagamba Kabudi amevipongeza vituo vyote vya redio kwa kazi nzuri ya
kuhabarisha umma wakati wote wa Mkutano wa Nishati wa Wakuu wa Nchi (Misheni
300) uliofanyika tarehe 27 – 28 Januari, 2025 jijini Dar es Salaam.
Profesa
Kabudi alitoa pongezi hizo wakati
akifungua mkutano mkuu wa watoa huduma za Utangazaji 2025 ulioanza Februari 13
na kufikia tamati Februari 14, 2025 jijini Dodoma ambao unafanyika katika maadhimisho ya siku ya Redio Duniani.
Alisema kupitia redio dunia ilifahamu kuhusu mkutano
huo muhimu ulioongozwa na mwana mazingira namba moja Mhe. Dkt. Samia Suluhu
Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
“ Kipekee nitumie
fursa hii kuvipongeza vituo vyote vya redio kwa kazi nzuri ya kuhabarisha umma
wakati wote wa Mkutano huo ambao likuwa ni wa muhimu,” alisema Kabudi.
Aidha, Kabudi amevipongeza vituo vya redio vinavyorusha vipindi maalum vya kuhamasisha utunzaji wa mazingira hasa Shirika la Utangazaji la Taifa (TBC) kwa kuwa kinara wa kuandaa vipindi vya kutoaelimu ya utunzaji wa mazingira kama vile: Jambo Tanzania (27 ya Kijani), Kampemi ya Pika Kijanja inayosimamiwa na BONGO FM na kipindi maalum cha kuhamasisha usafi wa Mazingira (Jicho la Mpita Njia) ambavyo vimekuwa chachu ya kuhamasisha utunzaji wa mazingira hapa nchini.
“ Kama
mnavyofahamu, mabadiliko ya hali ya hewa pamoja na tabia nchi ni ajenda muhimu
kitaifa na kimataifa ambayo inaathiri maisha ya mwanadamu siku hadi siku.
Mabadiliko ya tabia nchi yameweza kuathirimakazi ya watu pamoja na sekta ya
kilimo na ufugaji kwa kiwango kikubwa,” alisema Kabudi.
Alisema uzalishaji
wa mazao kwa ajili ya chakula umeathiriwa kutokana na mabadiliko ya misimu ya
mvua sambamba na ongezeko la joto duniani.
Alisema ili
wananchi waweze kuchukua tahadhari mapema Redio imekuwa ni chombo muhimu chenye
kutoa taarifa kwa Wananchi.
Aliongeza
kuwa utangazaji kupitia redio umekuwa na nguvu duniani kwa vile matangazo yake
hufikia watu wengi, kwa haraka na gharama nafuu kuliko chombo chochote cha Utangazaji.
Alisema moja
ya sababu ni unafuu wa kununua redio za kusikiliza ambapo wananchi wa hali ya
chini, hali ya kati na hali ya juu kiuchumi wanaweza kumudu kununua chombo hiccho.
“ Kwa sasa
redio nzuri zenye viwango vizuri hupatikana hata kwa bei ya Shillingi elfu kumi
na tano (15,000/=). Hivyo basi, kwa vile redio ni chombo kinachomilikiwa na
watu wengi duniani, na mimi pia niungane na kauli mbiu iliyotolewa na umoja wa
mataifa ya kuhakikisha kuwa tunakuwa na vipindi vya redio vinavyotoa taarifa za
mara kwa mara kuhusu mabadiliko ya hali ya hewa,” alisema.
Alisema Tanzania
kupitia Mamlaka ya Hali ya Hewa ni miongoni mwa nchi chache Afrika yenye vyombo
vya kisasa vya kutabiri mwenendo wa hali ya hewa nchini na duniani. Kupitia
jukwaa hili, nitoe wito kwa vituo vyetu vya utangazaji kutoa taarifa za mara
kwa mara kwa wananchi pamoja na wakulima kuhusu utabiri wa hali ya hewa.
Profesa
Kabudi akikumbusha umuhimu wa taaluma ya Utangazaji nchini na duniani kote
alisema utangazaji umekuwa ukitumika kuleta umoja miongoni mwa jamii na taifa.
Alisema pamoja
na jukumu la kuhabarisha, kuelimisha na kuburudisha, Serikali nyingi duniani
zimekuwa zikitumia vyombo vya habari na utangazaji kuwasiliana na Wananchi wake
kuhusu programu mbalimbali za kitaifa na kuhamasisha ushiriki wa Wananchi
katika miradi mbalimbali ya maendeleo.
Alisema redio
ni chombo muhimu sana katika kufikisha habari sahihi kwa wananchi ili kulinda
maadili na usalama wa Taifa lolote duniani.
Alisema utangazaji
usiozingatia weledi ulivyosababisha mifarakano, machafuko na mauaji kwenye
maeneo mbalimbali duniani.
Alisema Serikali zilizopo madarakani zimekuwa
zikitumia vyombo hivi kama nyenzo ya utulivu na kupata mrejesho na maoni mbalimbali
kutoka kwa wananchi kuhusu ujenzi wa taifa lao. Kwa kifupi utangazaji ni kiungo
muhimu kati ya Serikali na Wananchi katika kuhamasisha amani, mshikamano na
ujenzi wa Taifa.
Akijikita zaidi katika eneo hilo la utangazaji alisema huanzia kwenye maandalizi ya
vipindi kwa kutambua lengo la kipindi na kuhakikisha kuwa maudhui utakayopeleka
kwa hadhira itakayokusikiliza yanavutia na yameandaliwa kwa weledi mkubwa.
Alisema utangazaji
huendana na sauti inayovutia, yenye kutamka matamshi kwa ufasaha lakini vilevile
uwepo wa matumizi fasaha ya lugha unayotumia kutangaza.
“ Ni
matumaini yangu kuwa tutaendelea kutumia taaluma yetu kwakuandaa vipindi vyenye
tija kwa jamii na kuchochea maendeleo ya nchi ikiwa ni pamoja na kuzingatia
matumizi sahihi ya lugha yetu adhimu ya Kiswahili,” alisema Kabudi.
Akizungumzia
katika eneo la maudhui ya vipindi vinavyorushwa na vituo vyetu, alisema bado hatujafanya
vizuri sana na kueleza kuwa vipindi vigi
vina maudhui na ujumbe unaofanana na pia vimejielekeza katika utangazaji wa matukio
na michezo hususan muziki, badala ya kuelimisha.
“ Redio
nyingi hapa nchini bado hazijawa na vipindi vya kutosha vinavyotoa elimu
mbalimbali kwa jamii na badala yake zimejikita kwenye burudani za muziki na
mchezo wa mpira wa mguu. Pamoja na kuwa burudani ya muziki na michezo ni kitu
muhimu kwa jamii, bado hakujawa na uwiano mzuri kati ya vipindi vya kuelimisha,
kuburudisha na kuhabarisha< “ alisema Kabudi.
Alisema kimsingi,
uwiano huo uko kwenye Kanuni za Utangazaji, lakini bado vituo vyetu havizingatii
Kanuni na Sheria zilizopo. Kwa watu wanaoheshimu taaluma zao, sio jambo la
kiungwana mamlaka zinazosimamia Sheria na Kanuni kuwakumbusha kila wakati
nakuwachukulia hatua hivyo ni vyema kuheshimu taaluma kwa kufuataSheria na
Kanuni zilizowekwa.
Alisema Kauli
mbiu ya mkutano huo ni Wajibu wa vyombo vya Utangazaji kuelekea uchaguzi mkuu
wa 2025 na kuwa kauli hiyo
inatukumbusha
nafasi ya vyombo vyetu vya Utangazaji kwenye uchaguzi mkuu unaotarajiwa
kufanyika mwaka huu mwezi Oktoba.
“Naomba
nitumie nafasi hii kuvitaka vyombo vya Utangazaji kusimamiahaki na usawa katika
kuhabarisha taifa mwenendo wa kampeni za vyama vya siasa pamoja na kuzingatia
weledi na Kanuni za Utangazaji,” alisema Kabudi.
Mkurugenzi wa Habarika Media, Shabani Lulela (kulia) akibadilishani mawazo na mshiriki mwenzake wa mkutano huo.
Wamiliki wa Online TV wakiwa kwenye mkutano huo.
No comments