Breaking News

VYOMBO VYA UTANGAZAJI VYATAKIWA KUSIMAMIA HAKI NA USAWA WAKATI WA UCHAGUZI MKUU 2025

Wazizi wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Profesa Palamagamba Kabudi akihutubia wakati akifungua mkutano mkuu wa watoa huduma za Utangazaji 2025 wa siku mbili ambao umeanza leo Februari 13 hadi 14, 2025 jijini Dodoma.

..................................

Na Dotto Mwaibale, Dodoma

VYOMBO vya Utangazaji nchini vimetakiwa kusimamia haki na usawa na haki katika kuhabarisha  taifa mwenendo wa kampeni za vyama vya siasa pamoja na kuzingatia weledi na kanuni za utangazaji.

Ombi hilo limetolewa na Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Profesa Palamagamba Kabudi wakati akifungua mkutano mkuu wa watoa huduma za Utangazaji 2025 ulioanza leo Februari 13 na kufikia tamati kesho Februari 14, 2025 jijini Dodoma.

“Nitoe rai kwa washiriki wote wa mkutano huu kuhakikisha kuwa mnazielewa sheria na kanuni zote zinazosimamia uchaguzi mkuu nchini,” alisema Kabudi.

Alisema ni marajio yake kuona mada zote zitakazowasilishwa kwenye mkutano huo zitalenga kukumbushana  wajibu wa vyombo vya Utangazaji kuelekea uchaguzi mkuu ili  wananchi waweze kuelimika na kufanya maamuzi sahihi katika kipindi cha uchaguzi.

Kabudi alisema Sekta ya Utangazaji nchini na duniani kote imekumbwa na mabadiliko ya kiteknolojia ambayo yamefanya vyombo vya utangazaji wa kijadi  kuathiriwa kwa kiwango kikubwa kwenye uwekezaji walioufanya.

Alisema Serikali inayoongozwa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan inaendelea kufanyia kazi changamoto mbalimbali zinapitiwa na vyombo vya utangazaji.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) ambao ndio waandaaji wa  mkutano huo, Dkt. Jabiri Bakari alisema wameboresha sana eneo la huduma kwa wateja na kuwa kwenye kila kanda kuna mameneja na lengo lao ni kukua zaidi ili waweze kusonga mbele.

Alisema jambo lingine ni kuwa wanafanya kazi hiyo ili waendelee kufanya vizuri na kwa ustadi mkubwa ambapo alitoa shukurani kwa washiriki wa mkutano huo kwa michango yao.

Alisema Tanzania ni nchi yetu na kuwa vyombo vya habari vya mataifa ya wenzetu ya nje vimekuwa vikiandika habari za kizalendo zaidi kwa maslahi ya nchi zao .

“Teknolojia imeturahisishia kufanya kazi vizuri na kuchangia maendeleo makubwa ya kiuchumi lakini pale taarifa zinapokuwa na changamoto ni vizuri kuliangalia jambo hilo kwa maslahi ya nchi yetu,” alisema Dkt. Bakari

Dkt. Bakari aliomba kutumia simu za mkononi kwa ajili ya kufanya mambo ya maendeleo badala ya kuzitumia tofauti jambo ambalo linaweza kuturudisha nyuma.

Mtoa mada kwenye mkutano huo kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) Shule Kuu ya Uandishi wa Habari na Mawasiliano kwa Umma, Mhadhiri Abdallah Katunzi akizungumzia dhima ya vyombo vya habari vya utangazaji alisema ni kutetea maslahi ya umma, kusimamia amani na usalama wa nchi na kuwa ni gundi ya kushikanisha umoja wa nchi yetu.

Aidha, Katunzi alisema waandishi wa habari katika kipindi cha uchaguzi wanatakiwa kuandaa agenda mahususi badala ya kutegemea zaidi viongozi waliopo madarakani. Aliongeza kwamba sauti za wananchi ni muhimu sana kujumuishwa kwenye kazi za waandishi wa habari wakati wa uchaguzi.

“Mara nyingi sauti za wananchi wa kawaida imekuwa ni ndogo kutokana na waandishi kutowahoji na kutoa kipaumbele zaidi kwa wagombea,” alisema Katunzi.

Alisema katika kipindi hicho cha uchaguzi wagombea wanaume taarifa zao zimekuwa zikiandikwa zaidi kuliko za wagombea wanawake.

Washiriki wa mkutano huo wakichangia mijadala suala kubwa lililoibuka ni wanatasnia ya habari waliowengi hawana elimu ya kutosha na suala zima la kiuchumi nalo limetajwa kuchangia kufanya kazi pasipo kufuata kanuni na sheria.

Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA)Dkt. Jabiri Bakari, akizungumza kwenye mkutano huo.
Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo ambaye pia ni Msemaji wa Serikali, Geryson Msigwa akizungumza kwenye mkutano huo.
Mkuu wa Mkoa wa Dodoma,  Mhe. Rosemary  Senyamule, akizungumza kwenye mkutano huo.
Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Maudhui TCRA, Saida Muki, akizungumza kwenye mkutano huo.
Mkurugenzi Msaidizi wa Huduma za Sheria wa Tume Huru ya Uchaguzi (INEC), Cyprian Mbugano akitoa mada  kuhusu Uboreshaji wa daftari la kudumu la wapiga kura.
Washiriki wa mkutano huo kutoka Mkoa wa Singida wakiwa katika picha ya pamoja
Bloggers wakiwa katika majadiliano ya tathimini ya utekelezaji wa maadhimio ya mkutano mkuu wa utangazaji wa mwaka 2024.
Taswira ya mkutano huo.
Washiriki wakiwa katika mkutano huo. Kutoka kushoto ni Meneja wa Redio Harvest Time FM, Getson Sanga na kushoto kwake ni Mkurugenzi Mtendaji wa Misalaba Media ya Mkoa wa Shinyanga, Mapuli Misalaba.

Washiriki kutoka Tanzania Blogger Network (TBN) wakifuatilia mada zilizokuwa zikitolewa.
Mkutano ukiendelea.
WWaendeshaji wa Online TV wakiwa kwenye mkutano huo.
Mkutano ukiendelea.
Washiriki wa mkutano huo wakijisajili kabla ya kuanza kwa mkutano huo.
Washiriki wakibadilishana mawazo wakati wa mkutano huo.
Mkutano ukiendelea. Kutoka kushoto ni Kinara Lafuli kutoka Singida, Imani Ponera kutoka Site Digital, Edina Malecela kutoka Singidani Online TV na Mkurugenzi Mtendaji wa Cales Digital, Cales Katemana.
Mhariri Mtendaji wa Tanganyika Online TV, Hadia Khamis (kushoto) akiwa na Mhariri wa SM TV, Magreth Mkiga.
Taswira ya mkutano huo.
Mkutano ukiendelea. Kutoka kushoto ni Mkurugenzi wa Nicco Media TV, Mwandishi wa Habari wa Jambo Tv, Theophil Mbunda na Mkurugenzi wa Habari Faster, Emmy Mwaipopo.
Mkutano ukiendelea.
Washiriki wa mkutano huo wakifuatilia bada zilizokuwa zikitolewa.
Mwanahabari Mkongwe, Abdallah Majula akichangia jambo kwenye mkutano huo.
 

No comments