Breaking News

DKT BITEKO : MALENGO YA MATUMIZI NISHATI SAFI YA KUPIKIA HAYAWEZI KUFIKIWA BILA YA MWANAMKE

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Dkt Doto Biteko (kulia) akipata maelezo ya matumizi ya nishati safi ya kupikia alipotembelea mabanda wakati wa  kongamano la kuhamadisha matumizi ya nishati hiyo lililoandaliwa na Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO)

............................................

Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Dkt Doto Biteko, amesema, matumizi ya nishati safi ya kupikia hayawezi kufikiwa malengo bila kumshirikisha mwanamke.

Dkt. Biteko amesema hayo wakati wa kongamano la kuhamadisha matumizi ya nishati safi ya kupikia lililoandaliwa na TANESCO kuelekea maadhimisho ya siku ya wanawake duniani ambayo huadhimishwa machi 8 kila mwaka.

Amesema ajenda ya matumizi ya nishati safi ya kupikia inatekelezeka, na amewataka wanawake wote nchini kumuunga mkono rais Dkt Samia Suluhu Hassan ili kufikiwa yifikapo 2034 watu wote hususani wanawake wote nchini wawe wanatumia nishati safi ya kupikia kwa umeme.

Naye Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO), Mhandisi Gissima Nyamo- Hanga amesema Serikali imetia mkazo katika matumizi ya nishati safi ya kupikia na ni gharama nafuu na rahisi kwa matumizi.

Pia amesema lengo limelenga kuhakikisha Kila mwanamke wa Tanzania anapata fursa ya kutumia nishati safi ya kupikia kwa umeme.


Maelezo ya matumizi ya nishati safi ya kupikia yakitolewa.
Maelezo ya matumizi ya nishati safi ya kupikia yakitolewa.
Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO), Mhandisi Gissima Nyamo- Hanga akizungumza.
 

No comments