Breaking News

P0LISI NIGERIA YAWATIA MBARONI WAISLAMU 20 KWA KULA MCHANA MWEZI MTUKUFU WA RAMADHANI

Muonekano wa chakula kilichoandaliwa tayari kwa kuliwa

..................................................

Na Mwandishi Wetu 

IKIWA ni siku ya tatu tangu Waislamu wakiwa wameanza mfungo wa Mwezi Mtukufu wa Ramadhani Polisi wa Kiislamu katika jimbo la Kano, kaskazini mwa Nigeria wamewakamata Waislamu 20 waliokutwa wakila mchana hadharani wakati wa Mwezi Mtukufu wa Ramadhan ambapo pia Watu watano wamekamatwa kwa kuuza chakula huku Naibu kamanda wa Polisi Mujahid Aminudeen akisisitiza kuwa msako huo utaendelea mwezi mzima.

Aminudeen amesema hatua hiyo inalenga kudumisha heshima ya Ramadhan kwani Waislamu wanapaswa kufunga kuanzia alfajiri hadi jua linapozama pia ameeleza kuwa wale waliokamatwa tayari wamefikishwa katika Mahakama ya Sharia kwa ajili ya kuchukuliwa hatua za kisheria.

Mbali na hilo Polisi wa kiisalmu wa Hisbah pia wamewakamata Watu waliovaa mavazi yanayokiuka maadili ya Kiislamu wakiwemo waliokuwa na nywele zisizoruhusiwa na Madereva wa Bajaji waliowachanganya Abiria wa jinsia tofauti.

Mfumo wa Sharia umeendelea kutumika katika baadhi ya majimbo ya kaskazini mwa Nigeria kwa Waislamu tangu kuanzishwa kwake zaidi ya miaka 20 iliyopita na kutoa adhabu kwa wale wanaokiuka na kukamatwa wakila hakula mwezi mtukufu.

No comments